.

.
Tuesday, October 28, 2014

1:47 AM


Historia fupi sana ya Maisha yangu.
bertha ismail

Mimi Bertha Ismail mwandishi wa habari wa kampuni ya MCL Tanzania, pia ni mkurugenzi wa kampuni ya BIMO Media information iliyoko Arusha,  nilizaliwa tarehe 6-12- 1990 eneo la Ilboru jijini Arusha na kwa sasa naishi Kijenge juu.
happy birthday yangi ni decemba 6,

Nilianza elimu yangu ya msingi katika shule ya Olturoto iliyoko wilayani Arumeru mkoani Arusha mwaka 1999, nilihama shule hiyo mwaka 2001 baada ya wazazi wangu waliokuwa wananilea kutengana.

Mwaka 2002 nilihamia shule ya msingi Unga ltd na kuingia darasa la Tatu hadi nilipohitimu elimu yangu ya msingi hapo mwaka 2005.

Nilifaulu kuendelea na elimu yangu ya sekondari katika shule ya sekondari ya Kinana mwaka 2006 na kuhitimu elimu hiyo mwaka 2009.

Hata hivyo kutokana na ugumu wa maisha na malezi ya kuishi na mzazi wa kambo (baba) sikufanikiwa kuendelea na elimu ya kidato cha tano badala yake nilitafuta chuo cha kusoma.

Kwa kuwa tangu nikiwa mdogo nilipenda kazi ya Utangazaji sikuwa na chaguo lingine zaidi ya kuomba wazazi wangu waliokuwa wananilea kulipiwa ada ya kwenda chuo cha Uandishi wa habari na Utangazaji.

nimemaliza chuo naingia mtaani


Katika kipindi hicho chote sikuwa namjua wala kumfaham baba yangu mzazi ni yupi bali nilijua ni yule wa awali niliyekuwa namuona tangu nakua na baadae kuja kutengana na mama yangu na kuhama kijiji cha Olturoto na baadae alifariki hivyo nilijua ni baba yangu ndie aliyefariki na kuondoa matumaini ya kuja kuonana na baba yangu tena.

Kama ijulikanavyo maisha ya mzazi wa kambo mambo yalikuwa magumu sana hasa katika kukubalika katika mahitaji yangu mbele ya baba wa kambo hali iliyoleta ugomvi mkubwa kati ya baba yangu na mama yangu lakini kiubishi-ubishi niliamua kwenda kuchukua fom na kujiunga na chuo bila ada.

Kwa kutumia uongo uongo siku moja moja baba akisafiri mama huwa rafiki yetu hivyo nilitumia mda huo kutoa mahitaji yangu na mama kutimiza ambapo ada ya awali ililipwa na kuanza chuo hivyo angalau kuaminika lakini mambo yalienda hivyo hivyo kipindi ambacho mama hanielewi nililazimu kutumia uongo shuleni hadi kuhitimu masomo yangu ya cheti katika chuo cha Uandishi wa habari na Utangazaji Arusha (AJTC).

Ingawa nilikuwa na madeni na siku ya mitihani wanafunzi hawakuruhusiwa kufanya mitihani ya kumaliza chuo bila ada hivyo ilibidi nidanganye kadri nilivyoweza hadi kuruhusiwa kufanya mitihani na kuingia mitaani kuanza kutafuta habari na kuripoti redio five Arusha ambayo ilinisaidia kuanza kupata fedha kidogo kidogo ambazo nilipeleka shule kupunguza deni la Ada.

Katika kipindi hicho nilianza kusikia fununu kuwa baba yangu mzazi yupo hai na anaishi hapa Arusha hali ambayo sikuamini hadi nilipomuona ambapo nilitaka kujua historia ya kwanini hakutaka kunijua mwanae katika kipindi hicho chote cha mateso na mahangaiko lakini haikuzaa matunda ya kufahamu historia kamili bali fununu za mtaani.

Baada ya mda kidogo baba wa kambo akawa hataki nifanye kazi hali iliyopelekea kunifukuza nyumbani endapo nitaendelea na kufanya kazi kwa madai kuwa haoni faida ya kazi yangu, hivyo niliamua kutorokea kwa baba yangu mzazi ambapo hata huko nako mambo hayakuwa shwari kwa mama yangu wa kambo hali iliyopekekea mimi kutafuta namna ya kuanza maisha ya kupanga nyumba.

Kwa kutumia vijisent nilivyokuwa Napata katika kazi yangu ya kutafuta habari niliweza kupanga chumba cha udongo mwaka 2010 na kuanza maisha ambayo hata sikujua niyaendesheje.

Kwa bahati mbaya mkosi nao haukuniacha nyuma bali uliendelea kuniandama ambapo baada ya mda kulitokea maneno ya uongo katika ofisi hizo za Redio 5 Arusha kwa kuhujumiwa na hatimaye bila kusikilizwa niliamuliwa kufukuzwa kazi, kiukweli iliniuma lakini sikuwa na la kufanya.

Nilianza kusaka kazi kwa mara nyingine na Mungu nae hakuwa nyuma sana kunivuta mkono nilipopata tatizo, kwani nilibahatika kupata kazi katika kituo cha redio ya sunrise Arusha kama mtangazaji na mwandishi na baada ya mda  nikawa naandika gazeti pia moja lililoanzishwa na aliyekuwa mtangazaji  wa star TV, Anjelo Mwoleka liitwalo “kutoka Arusha” hali iliyonifanya niwe mwandishi mzuri hapa jijini Arusha.  

Baada ya mafanikio hayo na kumaliza deni hilo niliamua kujiandikisha shule na kuendelea na elimu yangu ya diploma ya uandishi wa habari na utangazaji Arusha huku maisha yangu mapya niliyoyaanzisha yakiwa mazuri kila kukicha kwani nilifanikiwa kumiliki godoro, kitanda. Na hata meza moja niliyokuwa naweka begi langu la nguo n.k.

Baada ya mda niliamua kuachana na utangazaji wa sunrise radio na kuhamia moja kwa moja gazeti hilo la kutoka Arusha ambapo hata hivyo baadae lilikuja kufa bila kuzikwa.
Mwaka 2013 nilihamia  gazeti la “Tanzania Daima” kama mwandishi wa michezo wa kujitegemea huku nikiwa nimeachana na redio sunrise kabisa.

Kama ijulikanavyo mwandishi wa kujitegemea ni kama mchezaji wa timu kubwa duniani, mwaka 2014 nilibahatika kununuliwa na kampuni ya “Mwananchi Communication Ltd” (MCL). Kama mwandishi wa michezo katika gazeti la mwanaspoti  ambapo pia habari zangu kwa sasa zinatumika hadi gazeti la Mwananchi na “the citizen”.

Pia mwezi wa 11 mwaka 2014 ni kuhitimu elimu yangu ya Diploma ya chuo cha uandhishi wa habari na utangazaji.

Kwa sasa mbali na uandishi pia nimesajili kampuni yangu kwa kutumia jila langu la “BIMO Media company” ambayo inajihusisha na kuandaa na kuratibu matukio mbali mbali ikiwemo la “shindano la uandishi wa insha kuhusu maswala ya utalii” pia matamasha na shoo mbali mbali za wasanii.

moja ya tuki la uandaaji wa tukio la uanshi wa insha iliyoandaliwa na kampuni ya BIMO Media information, hapa nikisoma risala mbele ya mdeni rasmi.

Mungu ameonekana kunipigania kila kukicha na kamwe sitasahau nilikotoka katika maisha yangu ambapo mbali na kuwa nina baba lakini bado sioni kama ninae bali ninae mama pekee ambae kwa sasa ameshaachana na baba yetu wa kambo na anafanya biashara zake katika vibanda vya soko kuu Arusha na mahusiano yetu kwa sasa ni kama mtu na rafiki yake siyo mtu na mzazi wake tena.
nikisindikiza moja ya wageni kama mkurugenzi wa kampuni kwenye tukio la ushindani wa uandishi wa insha
Naomba niwatie moyo watu wanaopitia magumu katika maisha yao kuwa Mungu yupo na anatenda hivyo kila mtu amtegemee yeye na kumuangalia kwa macho yote mawili kwani anatenda.

E- mail  berthaarusha@gmail.com                mediabimo@gmail.com

Mwisho……………

0 comments:

Post a Comment