.

.
Tuesday, February 2, 2016

4:28 AM
Arusha . Riba kubwa inayotozwa kwenye taasisi za fedha pamoja na ukosefu wa elimu ya biashara ya kuwawezesha wananchi kuwekeza fedha wanazokopa kwenye miradi ya uzalishaji mali imeelezwa kama chanzo cha kufilisi wakopaji na kufaidisha taasisi hizo.

Akizungumza mkoani Arusha kwenye mkutano mkuu wa kitaifa wa 26 wa wanachama chama cha ushirika wa Akiba na mikopo cha Tumaini SACCOS, mwenyekiti Neema Fredrick amesema kuwa asilimia kubwa ya matajiri duniani waliofanikiwa ni kutokana na mikopo lakini kwa sasa watu wengi wamekuwa wakifilisiwa na mikopo kutokana na kukopa fedha na kuwekeza kwenye miradi isiyozalisha.

“Matajiri wengi duniani wamefanikiwa kutokana na mikopo na kukopa kwa malengo ya kuzalisha, lakini kuna watu wengi pia wamelizwa na mikopo kwa kufilisiwa hata kile kidogo walichokuwa nacho kabla ya kukopa, na sababu kubwa mbali na riba kubwa inayotozwa kwenye taasisi za fedha kuwa chanzo lakini pia kukopa na kwenda kuwekeza kwenye mradi usiozalisha ni kikwazo hivyo ili kuepukana na hili tuepuke kukopa fedha bila kuwa na mradi wa uhakika siyo kukopa kwa anasa au kununua vitu vya kwenda na wakati”

Neema alisema kuwa kutokana na hilo, walianzisha SACCOS hiyo ya tumaini yenye miaka 24 sasa ambayo katika chama chao wameweza kuwa na fedha kiasi cha bilioni 4.4 kutokana na wanachama 787 ambayo lengo kubwa ni kuweka na kukopeshana wanachama kwa riba ndogo lakini baada ya kugundua wengi wanashindwa kulipa mikopo yao ambayo wanadai zaidi ya milioni 150 wameamua kutoka elim ya biashara sambamba na kuendelea kufuatilia madeni yao.

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha, msajili wa vyama vya ushirika mkoa ambae alikuwa mgeni rasmi, Nerei Kyara alisema kuwa uwepo wa vyama hivyo vya kuweka na kukopa kumesaidia kwa asilimia kubwa kupunguza malalamiko pamoja na kesi nyingi za mikopo sambamba na kusaidia wananchi kujiongezea kipato kutokana na kubuni miradi mbali mbali ya kufanya na kupunguza hata ukosefu wa ajira hasa wale wanaowekeza kwenye miradi mikubwa kama viwanda kwani haujiri pia.

“Kwa Arusha pekee tuna zaidi ya vyama 400 na kila chama kina wananchi wetu ambao wengi wako kwenye ajira rasmi na wengine hawako kwenye ajira lakini kutokana na hivi vyama wanaweza kujiendeshea maisha yao bila kuwa tegemezi kutokana na kukopeshana wanachokusanya hivyo kupunguza hata mzigo kwa serikali kuwa na idadi kubwa ya watu tegemezi hivyo kwa sasa watu wazingatie elim ya biashara ili kuweza kunufaika na vyama hivi badala ya kuviua”

“Zaidi ya yote niwatake muache kukopa kwa kuangalia mkumbo au wanawake kununua vitenge na wengine kununua magari kwani mwisho wa siku haitakusaidia zaidi itakufilisi hivyo jitahidini kukopa na kuwekeza kwenye miradi itakayowapa faida na kuwezesha kurejesha mkopo husika kwenye vyama hivi huku mkiachana na taasisi zinazotoza riba kubwa ili kukuza uchumi wenu binafsi na taifa kwa ujumla”

Kwa upande wake mmoja wa wanachama Journey Mwampalile amesema kuwa kwenye chama chao hadi sasa wanaweza kukopa kuanzia milioni moja hadi milioni 40 kwa mwanachama mmoja kwa kurejesha kwa asilimia ndogo ambapo kwa upande wake amefanikiwa kuanzisha miradi mbali ya ufugaji wa mifugo kama kuku, na maduka ya jumla mjini ambayo familia yake inaishi vizuri kwa kusomesha watoto na kujenga nyumba nzuri na kuondokana na kupanga chumba.

“Hata kama ukiwa na elim ya biashara lakini kukopa kwenye taasisi za fedha ni ngumu kukua kwa haraka kutokana na riba kubwa wanayotoa lakini uanzishwaji wa hivi vikundi vya SACCOS vinasaidia sana kutokana na mtu kukopa fedha aliyowekeza na baadae kukopa lakini pia mwisho wa siku kuna faida kutokana na vikundi hivyo ambayo wanachama hugawana kutokana na miradi ya chama tofauti na taasisi hizi faida ni za mmiliki wa taasisi pekee hivyo niombe watu wajiunge kwenye hivi vikundi wanufaike zaidi kwa kukuza uchumi kuliko kutegemea serikali kila kukicha kwa ajira”

Kwa mujibu wa Neema amesema kuwa kutokana na wanachama wao wengi kutokana na mashirika na world Vision na vision fund baadhi yao wanakaribia kufikia kustaafu hivyo kwa sasa wanafanya mpango wa wanachama wao kupata elim ya maisha baada ya kustaafu ambapo pia watawasaidia mitaji ya kuendeleza maisha yao.

Mwisho…………………

Next
This is the most recent post.
Older Post

0 comments:

Post a Comment