.

.
Friday, November 28, 2014

2:37 AM

Wanaharakati kutoka shirika la Kwieco la mkoani Kilimanjaro wakiwa katika maandalizi ya maadhimisho ya siku 16 za kupingaukatili wa kijinsia.
Maandamano ya kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yakipita katika mitaa mbalimbali ya mji wa Moshi.
Mkurugenzui wa shirika la KWIECO ,Elizabeth Minde (mwenye miwani myeusi) akiwa katika maandamano hayo.
Brass Band ya Chuo cha Polisi ikiongoza maandamano ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa kanda ya kaskazini yaliyofanyika mkoani Kilimanjaro.
Maandamano yakiingia katika viwanja vya manyema ambako maandamano hayo yalikomea na kufuatia na burudani mbalimbali sanjari na hotuba toka kwa mgeni rasmi.
Afisa habari wa shirika la KWIECO ,Veronica Ollomi akitoa maelezo juu ya utendaji kazi wa shirika kwa mgeni rasmi Mtumwa Mwako alipotembelea bana la shirika hilo .
Afisa habari wa KWIECO ,Veronica Ollomi akitoa zawadi kwa mgeni rasmi Mtumwa Mwako.
Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili,mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Mtumwa Mwako akipitia hotuba yake ,shoto kwake ni mwenyekiti wa kamati ya maadhimisho ya siku hiyo ,
Mkuu wa dawati la jinsia mkoa wa Kilimanjaro ,Mrakibu wa jeshi la Polisi ,Grace Lyimo pia alikuwa miongoni mwa washiriki wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ,Elizabeth Mushi akisoma risala mbele ya mgeni rasmi katika maadhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya manyema mjini Moshi.
Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa kanda ya kaskazini ,Dk Mtumwa Mwako akitoa hotuba yake katika maadhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Manyema.
Mratibu wa Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili kanda ya kaskazini ,Hilary Tesha (katikatika)akijadiliana jambo na baadhi ya washiriki katika maadhimisho hayo katika viwanja vya Manyema mjini Moshi.
Wanaharakati kutoka mashirika mbalimbali yanayopambana na vitendo vya unyanyasaji pamoja na ukatili wa kijinsia katika mikoa ya Kilimanjaro ,Arusha na Manyara wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi(hayupo pichan                                                                                                                                                                                                     chanzo libeneke la kaskaizni  

0 comments:

Post a Comment