.

.
Friday, April 24, 2015

12:39 AM
Bertha Ismail - Arusha

Vilabu  nane kutoka jijini Arusha zinatarajia kupimana uwezo katika mchezo wa Taekwondo katika ligi maalum  inayotarajiwa kutimua vumbi appril 25 mwaka huu katika viwanja vya Complex vilivyoko njiro jijini hapa kwa ajili ya kuchagua wachezaji watakaowakilisha mkoa katika mashindano ya kitaifa ya Mei mosi.



Vilabu vya Taekwondo vinavyojifua katika viwanja mbali mbali kwa ajili ya mashindano hayo ni pamoja na Tripple ‘A’, Naura, kili, Kijenge pamoja na Meru, Chishwea, M.S na AICC ambapo kila mchezaji anasaka nafasi ya kuchaguliwa kuunda timu ya mkoa itakayo wakilisha katika mashindano hayo ya mei mosi yatakayofanyika jijini hapa may 1 mwaka huu.



Akizungumza na gazeti hili, katibu mkuu wa shirikisho la mchezo wa Taekwondo Tanzania, Shija Shija alisema kuwa wametoa nafasi kwa vilabu mbali mbali kujiandaa na mashindano ya mei mosi itakayosaidia kuendelea kuwanoa wachezaji katika mashindano ya kitaifa baadae watakapokua wanachagua timu itakayowakilisha nchi kwenye mashindano ya Afrika hapo septemba kule Brazavile, Congo.



“Mashindano haya ni ya wazi kwa vilabu vyote Tanzania kushiriki ili kuwanoa zaidi wachezaji wao na tutaandaa mashindano mbali mbali kwa wachezaji kutoka ndani na nje ya nchi lengo ni kuwajenga wachezaji wetu kimashindano zaidi wazidi kuleta medali mbali mbali za kimataifa kama mashindano yaliyopita”



Mkurugenzi wa ufundi wa mchezo wa Taekwondo mkoa wa Arusha Richard Kitolo aliliambia gazeti hili kuwa wameandaa mashindano yao maalum ya ndani ili kuchagua wachezaji wazuri watakaoshiriki michuano ya mei mosi ambayo wao watatayatumia mashindano hayo  kuchagua timu ya mkoa itakayowakilisha katika mashindano ya kitaifa baadae.



“Sisi wenyewe tumeamua kuandaa mashindano yetu ya ndani kabla hayo ya mei mosi hayajafika ili kuanza mchujo wa wachezaji wenye uwezo mkubwa wa kupambana na mchujo wa pili tutaufanya kwenye mashindano hayo ya mei mosi kupata timu ya mkoa”



“Sisi mashindano haya kwetu ni mazuri na tutatumia kuchagua timu ya Mkoa,  lakini changamoto kubwa inayotukabili kwa sasa ni wachezaji wachache kutokana na wazazi kutoruhusu watoto wao kushiriki katika mchezo hasa wasichana hivyo tuwaombe wazazi wawaruhusu watoto kushiriki katika michezo kama hiyo kuwajenga kiakili na afya pia”

0 comments:

Post a Comment