.

.
Friday, June 6, 2014

7:25 AM

 ​​Kijana akiwa amembeba nyoka baada ya kucharangwa kwa mapanga akitoka naye nje ya uzio wa kanisa hilo
 Nyoka aina ya chatu aliyetolewa nyumbani kwa mfanyabiashara maarufu jijini Arusha Joseph Magesse akivutwa na wananchi kuelekea kwenye kanisa katoliki la karsamatiki eneo la Sakina jijini Arusha ambapo aliuawa kwa kucharangwa na shoka na wananchi wenye hasina na imani hizo za kishirikina
 MMOJA wawananchi akiwa ameshika shoka akiendelea kumchoronga chatu huyo
 Mabaki ya mwili wa chatu huyo baada ya kucharanwa
​​Nyumba yamfanyabishara ambapo alikutwa nyoka huyo na chini ni sehemu ya magari ya mfanyabiashra huyo

Katika hali isiyokuwa ya kawaida tukio la kuonekana kwa chatu mkubwa eneo la sakina. kata ya kiranyi lilivuta hisia ya wakazi wa jiji la Arusha na viunga vyake.

Tukio hilo la aina yake kutokea katika jiji hili lilitokea majira ya saa moja na nusu asubuhi wakati wenyeji wakiwa katika pilikapilika za kujiandaa kwenda kwenye shuguli za ujenzi wa taifa.

Chanzo cha habari hizi zinasema kuwa mmiliki wa chatu huyo ni Tajiri maarufu ambaye pia ni mfanyabiashara wa madini aitwae Joseph Magessa mwenyeji wa Musoma

Taarifa zinadai kuwa mmiliki wa chatu huyo leo alikuwa na safari ya kwenda Dar na familia yake ambapo huku nyuma alimuacha kijana ambaye anasadikiwa kuwa mtoto wa ndugu yake ambaye aliwafungulia geti na kutoka na gari

Chanzo hichi ambacho jina lake limehifadhiwa zinadai kuwa baada tu ya kijana huyo kurudi ndani alikutana na chatu huyo kitendo kilichomfanya atoke ndani kwa kasi huku akipiga kelele za kuomba msaada kwa majirani.

Baada ya kelele hizo majirani walitoka kusaidia ambapo kwa wakati huyo taarifa zilisha sambaa hali iliyofanya idadi ya watu kuwa wengi katika eneo hilo.

Mashuhuda wanadai kuwa chatu huyo alikuwa amefunikwa kichwani na kitambaa cha baibui huku kiwiliwili chake kikiwa kimefunikwa na kitambaa cheupe kilichokuwa kimeandikwa maandishi yanayo fanana ya kiharabu.

Wanachi kwa kuona hali hiyo waliamua kumburuza chatu huyo kuelekea katika Kanisa la KKKT Lutheran ambalo alipo mbali na eneo hilo.

Hata hivyo baada ya kufika hapo chanzo kilidai kuwa mmiliki wa chatu huyo hakuwa wa kanisa hilo hali iliyopelekea wananchi kumburuta tena kanisa la ST. Monica ambapo mmiliki alikuwa muumini wa kanisa hilo

Chatu huyo mwenye ukubwa wa futi 12 alipigwa na wananchi ambao walikuwa na hasira kali

Katika harakati za kumuua chatu huyo ambaye anakisiwa kufikia ulefu wa zaidi ya futi 12 zilidumu kwa takriban nusu saa, huku mashuuda wakisema kuwa joka huyo alizidi kuwa mkubwa kila alipopigwa au kukatwa.

Taarifa za ndani zinadai kuwa mmiliki wa chatu huyo alipopigiwa na mlizi wa nyumba hiyo juu ya tukio hilo alitoa kauli ya kutokuuwawa kwa chatu wake huku akidai kuwa huyo ni mama yake mzazi na kutoa onyo kuwa akikuta kauwawa atampiga mtu risasi

“Huyo chatu hawawausu naomba mumuache msimuuwe kama kuna mtu mama yake amemleta basi amuuwe

chanzo; jamii blog

0 comments:

Post a Comment