.

.
Friday, January 30, 2015

2:14 AM
Aliyekuwa mgombea mwenyekiti kupitia chama cha mapinduzi mtaa wa lolovono amejikuta akiwekwa chini ya ulinzi mkali wa mgambo wa kata ya sokon one baada ya kusaini posho ya halmashauri ya jiji la Arusha shilingi 20,000 bila kibali.
 
Mgombea huyo aliyejulikana kwa jina la Sudy Salum Kienda alikamatwa kufuatia barua enye tamko la mkurugenzi wa jiji la Arusha kumtaka mtendaji wa kata ya sokon one Meery Laurence kumtia hatiani mgombea huyo baada ya kubainika kusaini posho ya shilingi 20,000 kama mwenyekiti wa mtaa huo hali isiyo halali.

Akizungumza na mtuhumiwa huyo, Merry alisema kuwa january saba mwaka huu washindi wa kiti cha wenyeviti waliitwa kwenye semina elekezi ya utendaji wa kazi ambapo baada ya semina hiyo mtuhumiwa (Sudy )alihudhuria mkutano huo kimakosa na kusaini posho isiyokuwa yake hivyo kuichafulia jina halmashauri ya jiji la Arusha.

Akiwa chini ya ulinzi alipotakiwa kujibu tuhuma hizo sudy alikiri kuchukua fedha hizo huku akijitetea kuwa hakujua kama ni kosa ambapo hata hivyo aliamua kuirejesha mikononi mwa mtendaji huyo.

“Mimi sikuwa na nia ya kuiba hii hela kama mnavyonituhumu bali mimi nilifika pale nikimuulizia mtu aliyeniita ndio nikaambiwa saini hapo uchukue hela na mimi nikachukua sikujua ni ya wenyeviti maana nisingechukua kuepuka kunidhalilisha kiasi hiki.

Akizungumzia hali hiyo, mwenyekiti halali wa mtaa huo wa lolovono, Priscus Kwai (CHADEMA) alisema kuwa si mara ya kwanza kwa mwenyekiti huyo wa CCM kutaka kiti hicho kwa nguvu kwani awali siku ya kuapishwa pia alijaribu kumrubuni mtendaji huyo ili kuapishwa kama mshindi wa kiti hicho ambapo mtendaji alikataa.

“Huyu jamaa ameshika nafasi ya tatu lakini amekuwa akitaka kiti hiki kwa nguvu ambapo mwanzo alisambaza mtaani nimemuuzia kura na amenipa nyumba na gari na akaja kwa mtendaji alfajiri siku ya kuapishwa na kusema yeye ndio mshindi lakini mtendaji aligundua hilo na kunisubiri hadi saa tatu mda wa kuapishwa nikafika na akaona aibu akaondoka” alisema Kwai

“Baada ya kushindwa kuapishwa siku hiyo akaanza kunitishia maisha kuwa nitaona kama nitafika mbali, ambapo siku ya semina iliyofanyika golden rose iliyoendeshwa na mkurugenzi alienda na kujitambulisha yeye kama mwenyekiti halali wa lolovono na kusaini hela ambayo baadae baada ya kufuatilia ilijulikana kuwa amechukua hela bila halali na ndio tukapigiwa sim tukaenda kumkamata”

Aidha katika uchaguzi wa wenyeviti uliofanyika hivi karibuni, mtaa wa lolovono nafasi ya kwanza ilichukuliwa na Priscus Kwai (chadema) kwa kuwa na kura 802 na nafasi ya pili ikichukuliwa na Mosses Losingo (NCCR) kwa kura 333 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Suddy Salum Kienda wa CCM

0 comments:

Post a Comment