.

.
Tuesday, July 28, 2015

6:57 AM
Bertha Mollel,


Displaying IMG-20150706-WA0004.jpg
TIMU YA PANONE FC YA KILIMANJARO

 Ama kweli timu ya Panone fc ya mkoani Kilimanjaro imepania kupanda daraja msimu ujao wa ligi na hii ni baada ya Kocha wake mkuu Atuga Manyundo kuweka wazi ratiba ya mazoezi yake ikiwemo wiki mbili za mwisho kucheza mechi za kirafiki na timu kubwa za Simba, Mbeya city na Yanga.

Timu hiyo iliyoingia kambini kwa kujinoa ili kujiwinda na ligi daraja la kwanza msimu ujao chini ya kocha mkuu Manyundo alisema kuwa mara baada ya timu kuingia kambini yapo mapungufu mengi wameyaona ikiwemo Ubutu wa nafasi ya mlinda mlango, fowadi na kiungo hivyo kwa sasa anashauriana na benchi zima la ufundi kuanza usajili mapema.

“Nimeona nafasi butu ambazo nimekueleza ambazo kwa sasa tuko njiani kupiga hodi katika sehemu mbali mbali kusaka wachezaji watakaojaza hizo nafasi na kuwa kali kweli kweli lengo ni kutowaangusha wana Kilimanjaro katika msimu ujao lazima tupae hadi ligi kuu”

“Ila kikubwa kwa sasa ni kuwapa wachezaji waliopo mazoezi ya pumzi, kasi ya mpira na ukabaji na baada ya hapo ratiba yetu inasema tucheze mechi za kirafiki na timu kubwa kujua mapungufu, kama unavyojua sisi ni timu ya ligi kuu ijayo hivyo lazima tucheze na timu za ligi kuu na kama unavyojua Simba na Yanga ndio chaguo letu la kwanza”

“Ila kwa sasa macho na masikio yetu ni kucheza na vilabu vya Mbeya city, vilabu vya hapa Tanga kama Prison ili tujue wanavyocheza na sisi tujue mapengo yetu ni yapi na kuyajaza mapema maana huu mwaka kwetu ni kazi tu hakuna kuremba” alisema Atuga”

Kwa upande wake katibu mkuu wa kikosi hicho Augustino Mwakatumbula alisema kuwa kutokupanda kwa timu hiyo hawatakuwa na sababu yoyote kutokana na tiyari mazingira mazuri ya kupanda yamewekwa ikiwemo malazi, chakula na usafiri pamoja na posho nzuri za wachezaji .

“Yaani mimi niseme tu kuwa kama wachezaji wetu wasipotufurahisha kwa mwaka huu basi kwani hawatakuwa na sababu yoyote ya msingi ya kushindwa kushinda kutokana na mazingira mazuri tuliyowawekea na sasa tunaangalia kocha tu usajili anaoutaka ndio tuufanye hadi kieleweke”

Mwisho…………………

0 comments:

Post a Comment