.

.
Tuesday, January 14, 2014

11:41 PM
http://sundayshomari.files.wordpress.com/2010/11/kikwete10.jpgUTEUZI wa Mawaziri wapya kwenye Baraza la Mawaziri baada ya Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wa Mawaziri wanne Desemba 20, 2013 na mmoja kufariki dunia, umeanza kuibua maswali mengi miongoni mwa viongozi, wananchi. 



Rais Kikwete alitengua uteuzi wa Mawaziri hao kutokana na shinikizo la wabunge baada ya kuipitia Ripoti ya Kamati ya Bunge iliyoundwa kuchunguza athari zilizotokana na utekelezwaji wa "Operesheni Tokomeza Ujangili". 



Mawaziri ambao uteuzi wao ulitenguliwa ni aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi, Mifugo na Uvuvi, Dkt. David Mathayo, Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Bw. Shamsi Vuai Nahodha pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki. 



Nafasi nyingine ambayo iko wazi ni ile ya Waziri wa Fedha, ambayo aliyekuwa Waziri wake, Dkt. William Mgimwa, alifariki dunia Januari mosi mwaka huu. 



Macho na masikio ya Watanzania yapo kwa Rais Kikwete wakiamini kiongozi huyo, ana kazi ngumu ya kufanya uteuzi makini ambao utarudisha heshima ya Serikali hasa kwa wananchi walioathirika na operesheni hiyo. 



Wakizungumza na Majira ili kutoa maoni yao kwa sharti la kutotajwa majina yao gazetini, baadhi ya mawaziri ambao hawakuguswa na rungu hilo, walisema kuchelewa kwa Rais Kikwete kufanya uteuzi huo ni dalili nzuri ya kuteua mawaziri wenye sifa na uwezo wa kumsaidia katika wizara husika. 



Alisema suala la uteuzi wa nafasi nyeti za uwaziri, si kazi ndogo ndio maana amekaa kimya muda mrefu ili kuangalia nani anayeweza kutekeleza majukumu atakayompa ili kuleta matokeo mazuri kwa wananchi, Taifa kwa ujumla. 



Waliongeza kuwa, kazi kubwa ipo kwenye uteuzi wa Waziri wa Fedha ambaye uwezo wake utafanana na ule wa marehemu Dkt. Mgimwa kwani kifo chake ni pigo kubwa kwa Serikali iliyotambua uwezo wake na kumpa dhamana. 



"Dkt. Mgimwa alikuwa na uwezo mkubwa katika masuala ya fedha, aliweza kufanya mambo mengi ambayo kimsingi yameiletea sifa kubwa Serikali yetu ndani na nje ya nchi. 



"Imani yangu ni kwamba, Rais Kikwete ana washauri wazuri ambao watafanya kazi nzuri ambayo itakubalika na wananchi wote... tusubiri uteuzi wake," alisema mmoja wa Mawaziri wakati akitoa maoni yake. 



Kwa upande wao, baadhi ya wa n a n c h i wa l i o z u n g umz a na Majira, wamemshauri Rais Kikwete asikilize kilio cha wabunge ambao walishauri kuwajibishwa kwa mawaziri wengine ambao uwajibikaji wao si mzuri katika.



Serikali yake.
Walisema mbali na mawaziri ambao ametengua uteuzi wao, wapo watendaji katika wizara hizo ambao nao wanapaswa kuwajibishwa kwa kuondolewa katika nafasi hizo kwani kama wataendelea kuwepo, bado wataendelea kuwa kikwazo kwa mawaziri wapya watakaoteuliwa. 



"Mimi naamini CCM bado ina watendaji wazuri ambao wanaweza kupewa nafasi za uongozi na wakafanya kazi waliyopewa kwa ufanisi mkubwa. 



"Ni fursa nzuri kwa Rais Kikwete na wasaidizi wake, kukaa chini na kuteua viongozi ambao uteuzi wao utapokewa vizuri na wananchi... kati ya mawaziri ambao alitengua uteuzi wao, wapo ambao anaweza kuwarudisha ila si wote kwani ajali iliyowakuta, imechangiwa na wasaidizi wao," alisema Bw. Suleiman Sadif ambaye kitaaluma na mchumi. 



Akizungumzia suala la mawaziri ambao Kamati Kuu ya CCM iliwaita na kuwahoji, mjini Dodoma, Bw. Sadif alisema dhamira ya chama hicho si kutaka wafukuzwe kazi bali lengo ni kuwakumbusha viongozi hao watekeleze wajibu wao. 



Alimpongeza Rais Kikwete, kwa kuchukua uamuzi mgumu wa kutengua uteuzi wa Mawaziri wake kwani hiyo ndiyo demokrasia na uamuzi huo umeepusha malalamiko ambayo yangeweza kutolewa kwa Serikali kwani matokeo ya Operesheni Ujangili hayakuwa mazuri kwa Taifa. 



Uchunguzi uliofanywa na Majira umebaini kuwa, wananchi wengi wana hamu kubwa ya kuona Rais Kikwete akiteua Mawaziri vijana ambao utendajikazi wao umeonekana katika majimbo yao, Kamati za Bunge na kwenye mijadala mbalimbali yenye masilahi kwa Taifa.                                               

                                                                                                                 MAJIRA.

0 comments:

Post a Comment