.

.
Friday, May 29, 2015

3:27 AM
Mwanamichezo wa gofu za ridhaa (amacha) Prabvir Singh ameibuka kidedea katika michuano ya wazi ya siku mbili yajulikanayo kama “Northern province golf competition” na kufanikiwa kuwa bingwa wa mashindano hayo kwa mwaka 2015/2016.

Mashindano hayo ya wazi yaliyoandaliwa na chama cha gofu Tanzania, TGU (Tanzania gofu Union) kwa kushirikiana na Arusha gymkhana club (AGC) yalifanyika kwa siku mbili mwishoni mwa wiki ambapo Singh aliibuka mshindi wa jumla kwa kupiga mikwaju 141 na kufanikiwa kuwa bingwa na kuzawadiwa kombe kubwa.

Michuano hiyo iliyodhaminiwa na Benson Security System  pamoja na Sameer Parts ltd yaliweza kuwapa makombe pia mshindi wa daraja la kwanza Simon Travers aliyepiga mikwaju 149 akifuatiwa na Izak Wanyeche waliyepiga mikwaju 150.

Kwa daraja la pili Jugdish Ahluwalia “Chuchu” aliibuka mshindi kwa kupiga mikwaju 146 akifuatiwa na Kush Lodhia  149 huku daraja la tatu Rujvil Sohal akishinda kwa mikwaju 150 akifuatiwa na Alliabbas Somji aliyepiga mikwaju 151 wote wa Arusha.

Northern province golf competition yalishirikisha pia wanawake na Lina Francis wa Arusha kuibuka mshindi kwa kupiga mikwaju 148 na kwa watoto Jafari Omary wa TPC moshi kwa mikwaju 146 huku Habbib Yusufali (Arusha) akiibuka mshindi kwa upande wa wazee kwa kupiga mikwaju 168 na wote kupatiwa makombe madogo.

Zawadi za makombe pia zilitolewa kwa washindi waliovuka viwango (Cross winner) ambapo Abbas Adam wa Moshi aliibuka kwa kupiga mikwaju 154 akifuatiwa na Danniel Corpella kwa kupiga mikwaju 154 pia washindi wa siku ya kwanza Muzafar Yusufali aliibuka mshindi kwa mikwaju 72 na Minir Sheriff wa moshi alimfuatia kwa mikwaju 73.

Washiriki wa mashindano hayo 61 kutoka vilabu vya TPC na moshi club, Lugalo sambamba na Arusha walitakiwa na mgeni rasmi ambae ni mhazini wa gofu taifa Gelase Rutachibirwa kuwa wajitahidi kutafuta chipukizi wa mchezo huo watakaokuwa na viwango vizuri kuunda timu ya taifa ili kufanikiwa kushiriki katika mashindao mbali mbali ya kimataifa na kuiwakilisha nchi yetu.

Kwa upande wa mmoja wa wadhamini wa mashindano hayo kutoka Benson Security System, Nadeem Hussein alisema kuwa mashindano ya mara kwa mara kama hayo yanaweza kuwafanya wachezaji kupanda viwango na kuwa wataalam wa mchezo huo (Proffessional) na kupata ajira.

Mwisho………….

0 comments:

Post a Comment