.

.
Wednesday, July 3, 2013

6:54 AM
 
ZIARA ya Rais wa Marekani, Barack Obama hapa nchini, ‘imeivua nguo’ Serikali ya Tanzania, baada ya vyombo vya habari vya kimataifa kutoa tuhuma nzito za vitendo vya kikatili vinavyodaiwa kufanywa na vyombo vya dola dhidi ya raia.
Mweneyikiti wa Jumuia ya Madaktari nchini Dk Stephen Ulimboka, akiwa hospitali ya Muhimbili baada ya kutokea tukio la kupig
wa na kujeruhiwa vibaya na watu wasiofahamika hivi karibuni.  
Picha na maktaba ya www.jumamtanda.blogspot.com.
 
Hatua hiyo inayodaiwa kujaribu kufichwa kwa nguvu kubwa na baadhi ya watendaji wa serikali, imekuja kufuatia baadhi ya vyombo vya habari mashuhuri nchini Marekani, kuibua upya tuhuma za utekaji, upigaji na uuaji wa raia, waandishi wa habari na wanaharakati nchini Tanzania.

Moja ya chombo kilichoanika uovu huo, ni gazeti kongwe na mashuhuri linaloheshimika sio tu Marekani, bali na mataifa makubwa la New York Times, ambalo Julai 1, 2013, lilichapisha habari isemayo ‘Matukio ya udhalimu yaongezeka Tanzania, Kisiwa cha Amani Afrika’.
Mwenyekiti wa Jukwaa La Wahariri Tanzania (TEF), mwandishi na mwanahabari mzoefu, Absalom Kibanda aliyevamiwa na kujeruhiwa vibaya na watu wasiojulikana hivi karibuni wakati alipokuwa akirejea nyumbani kwake  Goba Punguni, Kata Ya Mbezi Juu akitokea kazini. 
Picha na maktaba ya www.jumamtanda.blogspot.com.

Habari hizo zilizoandikwa  na mwandishi maarufu wa habari za uchunguzi duniani, Nicholas Kulish zimeeleza tukio la kusikitisha la kutekwa nyara na kuumizwa vibaya kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Stephen Ulimboka, kama moja ya tukio baya ambalo linadaiwa kuwa na mkono wa serikali, ingawa Rais Jakaya Kikwete aliwahi kukanusha madai hayo.

Mwandishi huyo ameeleza namna Dk. Ulimboka alivyotekwa na kupakiwa kwa nguvu katika gari linaloaminika kuwa la moja ya vyombo vya usalama, kupigwa kwa kikatili kwa nyaya, kung’olewa kucha, na jinsi watesaji walivyoshauriana njia ya kumuua ikiwemo kumkanyaga na gari ama sindano ya sumu.

Mwandishi huyo, amemnukuu, Dk. Ulimboka akisema namna alivyowasikia watesaji wake, wakimwambia kuwa ‘atalipa yote aliyotenda’ na kumtaka asali na kumwomba Mungu wake, kwa sababu hataiona dunia tena.

Aidha, gazeti hilo limeieleza dunia kutekwa kwa waandishi wa habari na kuuawa  kikatili kwa mwandishi wa habari, Daud Mwangosi aliyeuawa na askari polisi akiwa kazini, katika Kijiji cha Nyororo, mkoani Iringa, mwaka jana.

Katika kuonesha uzito wa tuhuma hizo na namna wananchi wa Marekani wanavyotaka lishughulikiwe haraka, moja ya taasisi kubwa inayotetea waandishi wa habari duniani, yenye makazi yake jijini New York, ilimwomba Rais Obama kumkabili Rais Kikwete watakapokutana katika ziara yake iliyomalizika jana, juu ya matukio hayo na uhuru wa vyombo vya habari.

Kadhalika, gazeti hilo limeanika matukio mawili ya mashambulizi ya mabomu yaliyofanywa jijini Arusha kwenye Kanisa la Katoliki la Olositi na katika mkutano wa chama cha upinzani, (hawakukitaja) na kusababisha vifo vya watu saba.

Gazeti hilo pia limeeleza kwa kirefu namna shambulio la bomu la kurushwa kwa mkono lilivyotokea katika mkutano wa CHADEMA hivi karibuni huko jijini Arusha, na shutuma zilizotolewa na chama hicho dhidi ya Jeshi la Polisi kuhusika na kumtorosha aliyelipua bomu hilo.

Kadhalika, limenukuu msimamo wa CHADEMA wa kukataa kukabidhi kile kinachosemakana ‘mkanda mzima’ wa tukio hilo kwa polisi, hadi pale itakapoundwa tume huru kuchunguza tukio hilo.

Msimamo huu wa New York Times, wa kuichimbua Tanzania na kuyaanika maovu yake yote unaungwa mkono pia na magazeti mengi nchini Marekani, kama vile USA Today, ambalo nalo limechapisha habari zenye msimamo kama huo, likionesha wazi namna ziara ya Rais Obama ilivyotoa fursa ‘kumulikwa’ kikamilifu kwa matukio mabaya yaliyoikumba nchi.

Inadaiwa kwamba mara baada ya waandishi hawa wa Marekani kupata taarifa kutoka kwa Wizara ya Nje ya Marekani (State Department), juu ya ziara ya Obama hapa nchini, walianza kujipanga kufichua maovu  yanayotendwa na Serikali ya Kikwete.

Vyombo hivyo, vikafichua matukio mabaya yakiwemo uvunjwaji wa haki za kibinadamu, matukio ya matumizi ya nguvu kupita kiasi kwa upande wa polisi, kutokamilika kwa uchunguzi kwa matukio ya kihalifu na uhasama baina wa wafuasi wa chama tawala na wale wa upinzani.

Mbali na matukio hayo, vyombo hivyo, kinyume na vya hapa nchini ambavyo vimesifia ziara ya Obama, vimejikita kuibua uozo uliopo, likiwemo pia suala la kukithiri kwa uchafu katika Jiji la Dar es Salaam.


Chombo kingine kilichoandika mabaya ya Tanzania ni wavuti ya eTurbroNews ambayo inaandika kuhusu masuala ya utalii.
Watuti hiyo, Julai 1, 2013, iliibua habari za uchafu uliokithiri jijini Dar es Salaam, na kulitaja kuwa mojawapo ya majiji yanayosifika kwa uchafu likishika nafasi ya 12 duniani.

Habari hiyo imeushutumu uongozi wa jiji kwa kuamka dakika za majeruhi kufanya usafi na kujiuliza ilikuwaje wasubiri hadi ziara ya Obama kufanya kazi hiyo.

Aidha, habari hiyo imezungumzia kero ya kunguru weusi, na kushauri pengine ianzishwe kampeni ya watu kutoka nje kuja kuwawinda na kuwaangamiza kabisa, kama mchezo wa uwindaji, kwani sasa idadi ya kunguru hao waharibifu inazidi milioni moja. 
CHanzo, jumamtnada blog


0 comments:

Post a Comment