.

.
Thursday, October 31, 2013

1:31 AM



NA mwandishi wetu,
Maiti ya mwanamke Emeliana Kibuga(42) mkazi wa kijiji cha Kash Babati vijijini anaedaiwa kuuawa na askari wa hifadhi ya Tarangire octoba 16 inaendelea kusota katika chumba cha maiti katika hospitali ya wilaya ya Babati.
Hali hii imaetokana na ndugu kususia mwili huo kwa madai kuwa polisi wanawakinga wauaji wa ndugu yao huku wakishindwa kutoa taarifa sahihi juu ya mauaji hayo ambapo wamedai kuwa hawatauzika mwili huo ambapo kama hawatapokea taarifa hiyo basi wataupeleka mwili huo kwa mkuu wa mkoa ukakae hapo hadi kupata taarifa za mauaji ya ndugu yao.
Kwa mujibu wa ndugu wa marehem ambae ni mwenyekiti wa mtaa wa Unjej bwana Rashid Kijogoo alisema kuwa mume wa marehem alitekwa na askari wa hifadhi hiyo ya Tarangire octaba 14 saa nane za usiku nyumbani kwake kijijini hapo Kash na kumwacha mkewe lakini pia octaba 16  mkewe ambae kwa sasa ni marehem nae alitekwa na askari hao hao na kupelekwa kusikojulikana.
Alisema kuwa askari hao 6 wakiwemo wanawake wawili walifika katika kitongoji hicho na kumchukua marehem nyumbani kwake majira ya saa nne asubuhi kwa madai ya kwenda kufanya mahojiano nae na kumrudisha majira ya jioni huku akiwa chini ya ulinzi mkali wa askari hao wakiwa na  silaha za moto ambapo pia mwanamke huyo alionekana akivuja dam sehemu mbalimba;li za mwili wake.
Alisema kuwa baaada ya kufika nyumbani hapo askari hao walionekana kumhoji jambo marehem na kuondoka nae kwa mara nyingine ambapo kwa mara hii marehem hakuonekana tena hadi octoba 17 mwili wake ulipookotwa katika pori la hifadhi ya Tarangire huku akiwa amengolewa meno, na kutobolewa macho pamoja na kuvunjwa shingo.
Kijogoo alisema kuwa mwili huo unaodaiwa kuokotwa na askari wa hifadhi ya Tarangire ulipelekwa katika hospitali ya Wilaya, Mrara.
Kwa upande wake mtoto wa marehem aliyejulikana kama Christina Elias Kibuga alisema kuwa octoba 16 majira ya saa kumi jioni walikuja Watu sita wakiwemo wanawawe wawili waliovalia kiraia na wanaume wane, mmoja akiwa amevalia sare za jeshi la wananchi Tanzania (JWZT) ambapo walikuja na mama yao huku wakimhoji kwa ukali,
“Ilikuwa ni saa kumi jioni ikiwa ni siku mbili tangu baba atekwe usiku na siku hiyo nae mama alitekwa asubuhi na kurudishwa jioni na askari hao sita, mmoja akivalia nguo za jeshi walimleta mama yetu huku akiwa anavuja dam sehem nyingi na kumgombeza kuwa wawaonyeshe kitu alichosema kiko nyumbani, mama yetu alinyamaza tu ndipo walipomwambia tena kuwa kumbe hutaki bali umetusumbua bure kuja hadi huku, sasa leo utatutambua, wakaondoka nae tena hadi leo hatujamuona tena bali tunasikia kuwa ameuawa” alisema mtoto huyo huku akibubujikwa na machozi mfululizo.
Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa Manyara Akili mpwapwa alipohojiwa juu ya tukio hilo la mauaji, alikiri kuuawa kwa mwanamke huyo na kukanushwa kuuawa na askari hao kwa madai kuwa mwanamke huyo alikufa kwa mshutuko wa kuhojiwa.
Hata hivyo jambo hili limepingwa vikali na ndugu pamoja na majirani wa marehem huyo kwa madai kuwa mwili huo ulikutwa ukiwa na majereha mwili mzima iikiwemo kutobolewa macho, kuvunjwa shingo na meno kuonyesha kipigo kikali juu ya ndugu yao pia sehem za siri kuchubuka ambayo ni dhahiri ndugu yao alibakwa.
Nae Daktari wa hospitali ya wilaya ya Babati, Dr. Palagyo alithibitisha marehemu huyo kutobolewa macho, kuvunjwa shingo pamoja na meno sambamba na kuvuja dam sehem za siri hali iliyopelekea kifo chake.
Utekaji huo uliosababisha mauaji ya mwanamke huyo unafuatiwa na operesheni maalum ya kusaka majangili wanaojihusisha na uwindaji haramu wa meno ya tembo katika hifadhi mbalimbali za Taifa unaoendelea hapa nchini.



0 comments:

Post a Comment