.

.
Wednesday, October 23, 2013

5:29 AM
 
Mkutano wa siku mbili wa kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Arusha (RCC) Umeelezwa kwamba  Ziwa Manyara lipo hatari ya kutoweka kabisa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo uharibifu wa mazingira kunakotokana na kilimo pembezoni mwa mito kama juhudi za maksudi hazikuchulia kutunza mazingira yanayozunguka maeneo ya mito mbalimbali inayoingia ziwani humo.


Hali jii imetokana na kuongezeka   kwa shughuliza kibianadamu   hussani za kiuchumi na kusababisha pia ziwa manyara kujaa udongo na matope pamoja  uharibifu mkubwa  wa mazingira.


Akiwasilisha mada kuhusu  changamoto za uhifadhi katika hifadhi ya ziwa Manyara,Muikolojia katika hifadhi hiyo Bibi  Christina  Kiwanga amesema kukosana kwa utashi wa kisiasa ni changamoto kubwa katika kuliokoa ziwa hilo.


Bibi Kiwanga ametaja changamoto nyingine ni pamoja na kukosekana kwa mipango endelevu katika baadhi ya vijiji kuhusu umuhimu wa uhifadhi sanjari na elimu.


Muikolojia  huyo amewambia wajumbe wa kamati ya Ushauri ya Mkoa   wa Arusha kwamba  shughuli za Biandamu hususani za kilimo na za kiuchumi zimechangia kwa kiwango kikubwa  hifadhi hiyo kuwa katika hatari ya kutoweka.


Naye Meneja Ujirani Mwema makao makuu ya Tanapa BWANA Ahmed Mbugi amesema  umuhimu wa maeneo ya Mapito ya (SHOROBA) na mitawanyiko ya wanyama katika hifadhi amesema asilimia 80 ya Shooba  zilizokuwepo miaka ya nyuma zimetoweka kabisa.


Amesisitiza kwamba ni lazima  wananchi  walinde  uasilia  wa mapito ya  wanyama pori kutokana na umuhimu wa maeneo hayo

Mbungi amefafanua kwamba awali kulikuwa na  Maeneo ya SHOROBA yenye ukubwa  wa ekari 40,000 katika hifadhi za Arusha Kilimanjaro,manyara lakii maeeo haya yamepungua.


Aidha   amesisitiza kwamba wanasiasa wanachangia kuhujumu   maeneo haya ya uhifadhi kutokana na kukosekana  kwa kuchukuwa maamuzi mazito ya kuyalinda maeneo hayo kwa kuogopa wapiga kura hali inayoleta changamoto mbalimbali pindi wanapotoa taarifa za kulinda maeneo hayo.


Pia ameeleza kwamba asilimia 70 ya mapato yanayotokna na uhifadhi  yanatumika  katika usajidia  utekelezaji w amiradi ya kijamii ikiwemo ya afya,elimu, maji, na miradi ya barabara.


Amesema migongano baina ya wanyamapori na  binadamu inachangiwa na binadamu kuingilia maeneo ya mapito ya wanyamapori hivyo kuwakosesha njia za kupita hali inayoharibu mazingira.


Amesisitiza kwamba  hatua hii inasababisha kuathiri shughuli za utalii ambapo idadi ya watalii hupungua sanjari na shughuli za   uchumi kuathirika Mbali na  hali hii katika kipindi cha mwaka  1957/63 na 1987/`988 uoto wa asilimia   hususani misitu ulipungua kwa asilimia 13.5 wakati  maeneo ya kilimo yaliongezeka  kwa asilimia 10.9.


Aidha  maeneo ya ushorobo yaliyotumika kwa  shughuli za kilimo kati ya mwaka 1997/98 yaliongezeka  kati ya asilimia  8.35 hadi 11.41

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Lazaro Maasae yeye amesema kasi  ya ziwa manyara kuendeleoa kujaa ugondo na matope ni ya kasi zaidi

0 comments:

Post a Comment