.

.
Thursday, March 26, 2015

5:41 AM
BUNGE limepitisha rasmi Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya wa mwaka 2014, huku adhabu ya kifo kwa watakaokutwa na dawa hizo, ikishindikana kuingizwa kwenye muswada huo, isipokuwa mapapa na vigogo wa biashara hiyo, wameongezewa adhabu ya faini ya Sh bilioni moja na kifungo cha maisha.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge bado wameendelea kung’ang’ania kuwa sheria hiyo ijumuishe adhabu hiyo kali ya kifo kwa wafanyabiashara, mapapa au vigogo wanofadhili biashara hiyo, kwa kuwa madhara ya dawa hizo ni makubwa na yanaathiri zaidi vijana ambao ni nguvukazi ya nchi.

Akitoa majumuisho ya michango ya wabunge kuhusu hoja ya muswada huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama, alisema adhabu ya kifo haiwezekani kuingizwa kwenye sheria hiyo, kwa kuwa adhabu hiyo nchini iko kwenye makosa mawili pekee.

“Ni kweli Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo bado zinatoa adhabu ya kifo, lakini kwa mujibu wa sera iliyopo, adhabu ya kifo imeingizwa na kubainishwa kwenye makosa ya uhaini na mauaji pekee,” alisema Mhagama.

0 comments:

Post a Comment