.

.
Thursday, March 26, 2015

5:36 AM

"Hapo juzi Niliandika katika mitandao ya kijamii hasa nikizungumzia mchezo mchafu wa kisiasa unaofanywa na kambi ya ndugu EDWARD NGOYAI LOWASA. na nipende kurudia tena kuita kwamba anachoendelea kufanywa na edward lowasa kuwahadaa wananchi watanzania sasa aone kwamba tunatambua mbinu hizo chafu.\

Ndugu zangu watanzania baada yangu kuyasema haya edward ngoyai lowasa ameendelea kujitetea hasa akiandika katika ukurasa wake ya twiter na magazeti akisema amenipuuza sababu ya pili akisema mmi ni mchanga natakiwa niendelee kulelewa nikue, Naomba kumwambia lowasa udogo wangu mmi si katika Ukombozi wa maslahi ya Watanzania ila kama kweli Nitakuwa mchanga basi uchanga wangu nauona katika Kutokuwa mchafu, Mla rushwa, Mlaghai,Asiyewahadaa watanzania kwa mwamvuli wa dini,Lakini mwisho uchanga wangu ni kutowapikia ubwabwa washabiki wa siasa za Kumsafisha aliye mchafu.

Hayo niliyotaja tu ndio niko mchanga bado na kwa hayo edward ni mkongwe kupitiliza.
Mwisho namshauri edward aache maigizo na taifa hili watanzania wanahitaji kiongozi muadilifu na si anayewapa ubwabwa na kuwatumia basi kuja kwake wakiwa hawajashika tiketi za gari waliyosafiri nayo."
January Makamba.

0 comments:

Post a Comment