.

.
Monday, March 23, 2015

3:35 AM
Mwenyekiti wa tawi la yanga Arusha, Richard Elibariki Mollel amesema kuwa utafiti uliofanywa na wanachama wa yanga ikiwemo tawi la Arusha umeonyesha kuwa tangu yanga ianze kusajili wachezaji kutoka simba au waliowahi kuchezea samba timu yao ya yanga imekuwa ikifungwa na simba na shutuma kuangukia wachezaji hao.

Hivi sasa yanga inawachezaji zaidi ya watano tena wa kikosi cha kwanza waliowahi kuichezea simba na ukiangalia ndio chanzo cha yanga kugeuka vibonde kwa simba kikiwemo kipigo cha wiki iliyopita cha bao 1-0 na safari hii lawama zikiwaangukia Danny Mrwanda na kipa Alli Mustafa ‘Bartez’.

Mshabiki mkubwa wa timu ya Yanga mkoani hapa Ernest Manyilizu alisema kuwa tunaomba uongozi kama watatusikia warudie mfumo wa zamani wa kuwasajili wachezaji wakali kutoka timu zingine za mikoani kuliko kuelekeza macho yao kwa mkoa wa Dar-es-salaam hali ambayo inatutia aibu kufungwa na timu Simba kila mara kwa sisi kuwa vibonde wao.

“Mimi niseme tu kuwa uongozi wa juu wa Yanya utupe mahitaji yetu sisi mashabiki wao kwa kuachana na kusajili wachezaji waliowahi kutumika Simba kwani inawezekana wachezaji hao wakaja na mapenzi ya Simba kuitumikia Yanga hivyo ni rahisi kufanya urafiki wa kuwaachia ushindi na kama unavyojua ni bora kufungwa na timu zingine kuliko tufungwe na Simba hii ni aibu sana kutokana na sisi mbali na kuwa wakongwe wa soka lakini kumbuka ni watani wa jadi” alisema Ernest Manyilizu.

Mwanachama mwingine wa yanga Kefasi Filex “Sunguti” anasema “hata enzi za akina Nuruduni Bakari, Juma Kaseja na Athuman Idd Chuji,  yanga imekuwa ikifungwa kirahisi na wana Simba na sasa suluhisho ni kutema wachezaji wote waliowahi kuchezea Simba na kuepuka kusajili wachezaji toka kwa wapinzani wetu hao wa jadi, hivyo waangalie mpango mwingine wa kupata wachezaji wazuri ikiwemo hata kufanya mashindano maalum ya kusaka wachezaji au kutafuta nyota wakali katika timu hizi ndogo”

Mwisho………………………………..

0 comments:

Post a Comment