.

.
Tuesday, February 19, 2013

10:22 PM

Viongozi wa Chadema wakiwa wamekaa meza kuu katika mkutano wa Uzinduzi wa Chadema Kanda ya Kaskazini uliofanyika jana katika viwanja vya Ngarenaro Arusha.

Mwenyekiti wa Chadema Mh Freeman Mbowe akiongea katika mkutano wa ufunguzi wa Kanda ya Kaskazini.




Mwenyekiti wa taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, amekibebesha Chama Cha Mapinduzi (CCM) vurugu na mauaji ya kidini huku akiwaonya viongozi wa Chadema watakaoshiriki na kuhamasisha chuki dhidi ya dini nyingine kuwa watafukuzwa kwenye chama hicho asubuhi na mapema.
“Udini ni sera ya CCM, wamelikoroga, sasa tunataka walinywe,” alisema jana wakati akifungua mkutano wa viongozi wa majimbo 33 na mikoa ya Kanda ya Kaskazini inayojumuisha mikoa ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga, ikiwa ni sera yao ya majimbo.
Pamoja na kuwaonya viongozi, Mbowe pia aliwataka wanachama wa Chadema popote pale walipo wasishiriki kuwabagua wenzao kwa imani ya dini bali waheshimu imani za watu wengine.
Aidha Mbowe alisema; “Chadema inalaani vikali mauaji ya viongizi wa dini yanayotokea maeneo mbalimbali nchini…tunaitaka CCM na serikali yake kuwajibika dhidi ya mauaji hayo.”
“Kuona kiongozi wa dini akimwagiwa tindikali, akipigwa na hata kuuawa kwa sababu za kidini sio mambo ya kujivunia hata kidogo…CCM ndiyo iliyokuwa ikilea udini na hapo ndipo ilipotufikisha…tunataka CCM na serikali yake iwajibike kwa hilo.”
Alisema Mkristu hana haki ya kumhukumu Mwislamu na wala Mwislamu hana haki ya kumhukumu Mkristu, hivyo Chadema kimeamua kuchukua hatua kali dhidi ya mwanachama ye yote bila kujali wadhifa wake atakayehamasisha chuki za kidini.
Alisema sera ya udini iliaasisiwa na CCM kama mbinu yao ya kuwafanya waendelee kubakia madarakani lakini hali inavyoonekana sasa inatisha amani na umoja wa taifa.
 

0 comments:

Post a Comment