.

.
Tuesday, February 5, 2013

12:46 PM
                                    
 Pichni Mtoto Fransi Mgogi akipewa huduma ya kwanza na Muuguzi wa zamu Hirido Mligo katika kituo cha Afya  Migoli.

 Punda aliyefanya unyama  huo huyo hapa (picha na habari na  Saidi Ng'amilo )
  MTOTO ang'atwa na  punda mkono  wake  wakati akicheza jirani na  punda  huyo katika  eneo la Migoli  Mtera  wilaya ya Iringa vijijini mkoani Iringa .
 
Tukio hilo  limetokea leo  majira ya saa  12;30 jioni katika kijijini  Migoli baada ya Punda huyo kumng;ata mtoto mdogo wa kiume mwenye miaka 6 wa kijiji hicho .
 
Punda huyo akiwa mitaani akizurula bila utaratibu ilivyo kawaidayao katika maeneohaya  alikutana na Mtoto Fransi  nakumkamata mkonowake wa kushoto kwa kinywachake na kumning’iniza juu akikimbianae mpaka wananchi walipo msogelea kwa mayowe na kipigo akamuachia.
 
 Baba wa mototo Ndg Francis  Mgogi akizungumza na muandishi kwamasikitiko makubwa alisema tukiohili nilaajabu lakini anawasiwasi na haliya huyo Punda ingawa  kunakawaida ya Punda kuzagaa bila kujulikana mwenyenao nahuwezi muuliza mtu.
 
Akiwa katika kituo cha Afya Kope kataya migoli alipopelekwa mtotohuyo alipokelewa na Muuguzi wa zamu Hirida Mligo  ambae alipokuwa akimpahuduma kwa bahati mbaya Umeme ulikuwa umekatika toka saa tisa jionihiyo kukapelekea kuwa na giza katika chumba cha Upasuaji.
 
Ilimbidi muuguzi huyo kutumia taa ya mionzi ya jua ambayo ilikuwa na mwangamdogosana akiombamsaada wa kumulikiwa anapomsafisha eneolililo jeruhiwa akagunduo shimokubwa lililo tokana na jino la Punda likionyesha Mfupa wa nyuma ya mkono juu ya Kiwiko.
 
Haliiliomfanya   muuguzi  kumshauli Mzazi akisha mpatia sindano ya kinga inabidi amkimbize mjini jambolililo Mshitua mzazihuyo alisikika akisema uwezowa kukodi Gari hana itambidi alale apande Basi asubuhi kumpeleka Hospitali ya Mkoa wa Iringa  kwa matibabu zaidi.
 
Kwabahatimbaya mudawotehuo Dr wa zamu alikuwa hajafika ingawa muuguzi wa zamu alimtuma mlinzi akamuite.
 
Akizungumza na muandishi Dada mmoja Esta John mkazi wa kijiji Migoli alisema Pundahuyo kaisha fanya matukio zaidi ya hilo alishamuuma mbwa na kuuwa kabisa siku za nyuma na janayake amemuuwa Bata kwa kumkata shingo.
 
Juhudi za muandishi kumpata Dr wa mifugo kuthibitisha Uzima wa Punda huyo hazikufanikiwa alipofika nyumbani kwake na kupewa nambaya Simu ambayo alipompigia haikupokelewa.   
                                 

0 comments:

Post a Comment