.

.
Tuesday, February 19, 2013

5:40 AM
Kiongozi wa kanisa katoliki Tanzania, Muadhama Kadinali Polycarp Pengo
 
KIONGOZI wa kanisa katoliki Tanzania, Muadhama Kadinali Polycarp Pengo amewataka wakristo kutolipa kisasi kufuatia kuuawa kwa Padri Evarist Mushi huko Zanzibar.

Amesema wakristo kulipa kisasi hakutawasaidia kwani ni kinyume cha mafundisho ya dini ya kikristo na sheria za nchi. Kadinali Pengo ameitaka Serikali  kuwa makini na watu ambao wanataka kuivuruga amani ya nchi kwa kisingizio chochote kile.

Kiongozi huyo amevitupia lawama vyombo vya usalama wa nchi kwa kutochukua hatua za tahadhari kwani kulikuwa na ishara ya uhalifu kupitia vipeperushi vilivyosambazwa huko Zanzibar.

0 comments:

Post a Comment