.

.
Tuesday, March 18, 2014

12:34 PM
Na Bertha Mollel - Arusha


Timu ya AFC ya Arusha wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa mkoa wa Arusha baada ya kuifunga timu ya laibon ya longida kwa magoli 9-1 katika mchezo wa mwisho wa hatua ya sita bora ya ligi ya mkoa wa Arusha.

Ushindi huo umeifanya Timu ya AFC kufikisha jumla ya pointi 11 sawa na mana FC lakini afc ikanufaika na idadi kubwa ya magoli kwa kuwa na magoli 17 ya kufunga na matatu ya kufungwa wakati mana wao wana magoli tisa ya kufunga na hawajafungwa goli hata moja

Katika mchezo huo uliofanyika kwenye uwanja wa kumbukumbu ya sheikh amri abeid kaluta mjini hapa hadi mapumziko afc walikuwa wanaongoza kwa magoli 4-0 yaliyofungwa na Eriki Daudi  na Jamal aliyefunga mawili na Mgona Kifaru

kipindi cha pili afc walikuja na nguvu zaidi na kujipatia magoli matano zaidi yaliyofungwa na Alidina Hashim kwa penalt,Samson Mwalukwa,Abas Nkuba na Jamal tena aliyefunga magoli mawili.

nafasi ya pili imeshikwa na mana FC ,wa tatu Arusha meat,wa nne flamingo,nafasi ya tano imeshikwa na suye na timu iliyoshika mkia ikiwa ni timu ya laibon ya Longido.

mgeni rasmi katika mchezo huo alikua mkuu wa wilaya ya Arumeru Nyirembe Munasa Sabi aliwazawadia kombe afc ambao sasa watauwakilisha mkoa wa Arusha katika ligi ya kanda ngazi ya taifa

kwa kutwaa ubingwa huo afc imezawadiwa shilingi million 50 kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo ambaye aliahidi kutoa kiwango hicho kwa timu yeyote itakayotwaa ubingwa wa mkoa huku wadau wa michezo wa mkoa wa arusha wakiahidi kuiunga mkono timu hiyo ili ipande daraja hadi kufikia ligi kuu kama zamani.

Munasa alisema kuwa kiwango cha wachezaji kinaridhisha ila kwa sasa bado upande wa makocha bado hawatoshi ambapo ameahidi kuanza mchakato wa kutafuta makocha kutoka nchi za nje watakaokuja kuwanoa makocha wa Arusha.

0 comments:

Post a Comment