.

.
Saturday, May 17, 2014

4:12 AM
BAADHI ya wananchi wilayani Hanang’, Manyara wameanzisha biashara ya uuzaji vyuma chakavu na kusababisha uharibifu wa miundombinu hasa ya barabara.
Mkuu wa Wilaya ya Hanang’, Christine Mndeme, alibainisha hayo juzi alipozungumza kwenye baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya na kueleza kuna watu wameanzisha biashara hiyo ambayo imekuwa ikichangia uharibifu  wa miundombinu.
“Biashara ya vyuma chakavu imeanza kushamiri mjini kwetu, serikali inahangaika kuboresha miundombinu ya barabara, watu wanaiharibu kwa kung’oa vyuma katika maeneo kadhaa na kwenda kuuza. Tusaidiane kudhibiti hali hii, ili kukomesha uharibifu wa miundombinu,” alisema.
Mndeme alibainisha kwamba kuna watoto walioanzisha zoezi la kulenga shabaha kwenye nguzo za umeme, jambo ambalo ni hatari kwao na kwa mji mzima kutokana na athari za umeme zitakapotokea pindi wanapolenga shabaha vikombe vinavyoshikilia kwenye nguzo hizo.
Mbali na hilo, alihimiza suala la usafi na kusema mazingira ya mji huo ni machafu hasa maeneo ya katikati ya stendi ambapo mapipa ya kuhifadhia takataka yanajaa bila wahusika kuyafanyia usafi na kusababisha harufu mbaya.

0 comments:

Post a Comment