.

.
Sunday, May 11, 2014

10:14 PM
KINDA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abdulaziz Abubakari ‘Dogo Janja’, amesema kwa sasa atakuwa anafanya kazi zake za muziki jijini Arusha kutokana na mashabiki wengi wa Dar es Salaam kutomthamini.
Dogo Janja, alisema jana kuwa kuanzia sasa akitaka kufanya kazi zake atasafiri kwenda Arusha maana amegundua kama ndiko anakokubalika zaidi kuliko mikoa mingine.
“Sio kwamba sitafanya kazi kabisa Dar es Salaam, nitafanya, lakini asilimia nyingi nitazifanyia nyumbani maana kule nathaminiwa sana, huku dharau nyingi na watu tunachukuliana poa tu, lakini mimi nataka kufanya kazi zangu nyumbani na sio Dar es Salaam tena.
“Unajua mwenye asili haachi asili na akiacha asili hana akili, nyumbani nakubalika sana hivyo sina budi kwenda kuwafurahisha mashabiki pamoja na familia yangu,” alisema msanii huyo mwenyeji wa Arusha.
Dogo Janja ni kati ya wasanii ambao wanatamba kupitia kazi zao kutokana na uwezo walionao pamoja na kukubalika katika jamii inayowazunguka

0 comments:

Post a Comment