.

.
Wednesday, May 28, 2014

4:43 AM

Rachel HauleIKIWA zimepita siku chache tangu msiba wa mwigizaji na muongozaji filamu za Kibongo, Adam Kuambiana, mwigizaji mwingine, Rachel Haule ‘Recho’, amefariki dunia jana asubuhi.
Inaelezwa kifo cha Recho kimesababishwa na uzazi, ambapo alijifungua kwa upasuaji na mtoto kufariki. Kutokana na hali hiyo, alilazwa chumba maalumu cha uangalizi ‘ICU’ na baadaye kufariki dunia.
Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steve Mengele ‘Steve Nyerere’, alisema msiba upo Sinza kwa Remmy jijini Dar es Salaam kwa mjomba wa marehemu.
Hata hivyo, Steve alisema wapo katika mchakato wa kuiomba familia kumzikia hapa jijini Dar es Salaam, ili wadau mbalimbali wa filamu waweze kushiriki mazishi yake, badala ya kwenda Songea kama wanavyotaka.
Recho alianza rasmi kuingia katika sanaa ya maigizo mwaka 2009, katika kikundi cha Mburahati, kabla hajajiingiza rasmi kwenye uigizaji wa filamu.
Moja ya sifa zilizomfanya kujulikana, ni tabia ya kupendelea kuvaa nguo fupi, jambo ambalo alipohojiwa, alisema zinamfanya ajisikie huru na amani pindi anapofanya shughuli zake.

0 comments:

Post a Comment