.

.
Friday, March 29, 2013

11:38 PM



















Nairobi, Kenya
JOPO la Majaji sita nchini Kenya leo wanatarajia
kuweka historia mpya watakapokuwa wakiandaa uamuzi wa uhalali wa uchaguzi Mkuu uliofanyika Machi 4 mwaka huu.
Watu mbalimbali ndani nan je ya nchi hiyo watafuatilia kesi hiyo iliyofunguliwa na Mgombea wa Muungano wa CORD Raila Amolo Odinga ya kupinga matokeo ya Urais yaliyomuweka Uhuru Kenyatta madarakani.
Uamuzi wa Jopo la Majaji sita wa Mahakama ya Juu nchini humo ndiyo itakayo maliza ubishi kama Kenyatta ataendelea kubaki Ikulu ama atarudi kwenye Uchaguzi huo. 
Huu ni uchaguzi wa kwanza nchini Kenya kupingwa Mahakamani chini ya Katiba Mpya ya nchi hiyo.
Odinga alifungua kesi katika Mahakama hiyo baada ya kudai kwamba haridhiki na matokeo ya Urais kutokana na wizi wa kura uliofanywa na Mgombea wa Jubilee Uhuru Kenyatta.

0 comments:

Post a Comment