.

.
Thursday, March 14, 2013

12:53 PM
  Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa
 ---
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa ametoa salamu za pongezi kwa Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis I kwa kuchaguliwa kuliongoza Kanisa hilo Duniani.

Lowassa ametuma salamu hizo kwa Papa kupitia ukurasa wake wa Facebook na pia ametoa pongezi kwa Wakatoliki wote Duniani kwa kumpata Kiongozi huyo ambaye kiasili na jina lake ni Mt. Francis ni mtu wa kawaida.

Huu ndio ujumbe Kamili aliyouandika Ndugu, Edward Lowassa katika Ukurasa wake huo:-

“Hongera Cardinal Jorge Mario Bergoglio kwa kuchaguliwa kuwa Pope Francis I,

Na pia hongera wakatoliki wote duniani zaidi ya bilion 1 kwa kumpata Kiongozi ambaye kiasili na jina alilolichagua la Mt Francis ni mtu aliyeishi maisha ya kawaida na ya kuwapenda masikini katika maisha yake yote ya uitumishi.

Naamini sasa dunia mpya ya watu masikini kupata tumaini la maisha imezaliwa, na kwa pamoja tuungane kumpongeza na kumtakia mafanikio mema kiongozi wetu mkuu wa Kanisa katoliki duniani.

Na pia Roho mtakatifu amwongoze katika kuzikabili changamoto za kanisa duniani kote.” Alimalizia Lowassa katika Ujumbe huo.

ASANTENI SANA.

0 comments:

Post a Comment