.

.
Thursday, March 28, 2013

3:08 AM

Huyu  ndie mtuhumiwa wa mauawaji ya Mwangosi (kulia)
 
MTUHUMIWA  wa kesi ya mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa chanel ten mkoani
Iringa, marehemu Daud Mwangosi ambae  upelelezi  wake bado  kukamilika anatarajiwa kufikishwa mahakamani  leo machi 28  kwa mara nyingine .
 
Kesi  hiyo  yenye mvuto mkubwa kwa  wakazi wa mkoa  wa Iringa na watanzania pamoja na dunia kwa ujumla imekuwa ikiendelea kutajwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa  wa Iringa na hadi sasa ni zaidi ya mara 10 mtuhumiwa huyo amefikishwa mahakamani kwa staili mbali mbali .


Katika  kesi hiyo ambayo mtuhumiwa  wake ni  askari  wa  kikosi  cha kutuliza ghasia mkoa  wa Iringa
(FFU) Pasificus Cleophace Simon (23) mwenye namba G 2573 mbali ya  wananchi  wengi  kuwa na mvuto na kasi hiyo ila kwa upande wa jeshi la polisi mkoa  wa Iringa bado  askari wamekuwa  wakimficha mtuhumiwa  huyo ili asipigwe  picha na  wanahabari .

0 comments:

Post a Comment