.

.
Friday, March 29, 2013

10:48 PM

    Hiki ndicho kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15.
    Winchi likiokoa mabaki ya moja ya gari lililoangukiwa na kifusi.
VIDEO IKIONYESHA JINSI JENGO LILIVYOANGUKA JIJINI DAR LEO.
   Rais Jakaya Kikwete (katikati) akiangalia hali ya uokoaji inavyoendelea.
    Mkuu wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, akitoa maelekezo ya jinsi ya kuondoa kifusi eneo la tukio.
   Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki (katikati) akifuatilia shughuli ya uokoaji.
    Watu mbalimbali wakiondoa kifusi.
   Askari aliyejuu ya farasi akihakikisha usalama eneo hilo.
   Baadhi ya watu wakilisukuma gari ambalo pia lilikuwa kwenye ajali hiyo.
  Mama Salma Kikwete (kulia) na Rais Kikwete wakiangalia kifusi.
   Kijana aliyenusurika katika ajali hiyo akinywa kahawa.
LEO majira ya saa mbili na nusu asubuhi Watanzania wameingia kwenye vilio baada ya jengo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es Salaam, kuanguka na kuwafunika watu waliokuwa eneo hilo na kusababisha wengine kupoteza maisha. Mpaka sasa haijajulikana idadi kamili ya watu waliokuwemo ndani yake,.

  Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea, huku nondo nyembamba zikionekana na kuacha maswali miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo.
  Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea.
 Jitihada za kuwaokoa watu zikiendelea.

Taarifa  zilizotufikia mchana  huu zinadai  kuwa  idadi ya majeruhi  wa ghorofa  lililoporomoka  jijini Dar es Salaam imefikia  18  wakati  watu  wanne  wanadaiwa  kupoteza maisha na jitihada za uokoaji  bado  zinaendelea .

0 comments:

Post a Comment