.

.
Saturday, September 28, 2013

10:29 PM

Wakenya walimaliza siku tatu za maombolezi Ijumaa.

Imetimia juma moja kamili tangu jengo la maduka mjini Nairobi kushambuliwa na watu wengi kuuwawa.

Watu wenye silaha walivamia jengo la Westgate, magharibi mwa Nairobi, na kwa siku kadha waliendeshana mbio na vikosi vya usalama huku wakifyatua risasi na kuuwa wateja waliokuwamo kwenye maduka hayo, pamoja na watoto.

Hadi sasa inajulikana kuwa watu 67 waliuwawa.

Mamia ya watu walikuwemo kwenye jengo la biashara washambuliaji walipoanza uvamizi Jumamosi iliyopita.

Mwandishi wetu mjini Nairobi anasema moto bado unatokota sehemu ya jengo hilo.

Alama za risasi zinaonekana kwenye kuta - matokeo ya mapambano baina ya jeshi la Kenya na wapiganaji.

Zana nzito zinatumiwa kunyanyua kifusi cha saruji, na hapo ndipo itajulikana iwapo washambuliaji waliuwawa na mateka wangapi zaidi walikufa.

chanzo: BBC

0 comments:

Post a Comment