.

.
Sunday, September 8, 2013

12:11 AM

Na mwandishi wetu-Arusha

Zaidi ya watoto 30 wenye umri chini ya miaka 15 wamebakwa na kulawitiwa kwa nyakati tofauti mkoani Arusha kuanzia mwezi januari hadi September mwaka huu.

Akizungumza na gazeti hili katika hospitali ya mkoa wa Mount Meru, kwa niaba ya mganga mkuu wa hospitali hiyo, daktari Bura Eliza alisema kuwa vitendo vya kinyama dhidi ya watoto wenye chini ya umri wa miaka 15 vinazidi kushamiri siku hadi siku huku wahusika wakishindwa kuchukliwa hatua kali za kisheria.

Alisema kwa mwaka huu watoto zaidi ya 30 wamebakwa na wengine kulawitiwa kwa nyakati tofauti  huku hali hiyo mbali na kuwaathiri kiafya lakini pia huwaathiri watoto hao kisaikolojia.

“Vitendo vya ubakaji kwa watoto wadogo vimekithiri kiukweli kwani kwa sasa kwa mwezi tunaweza kupokea hadi watoto 5 ambapo tukiangalia kuanzia januari hadi leo September watoto 32 wamebakwa na hapo bado hatujamaliza mwezi huu” alisema Eliza na kuongeza,

“Mbaya zaidi watoto hao wanaobakwa na kulawitiwa bila kujali jinsia kuna baadhi yao hasa wasichana wanafanyiwa vitendo hivyo kwa wakati mmoja yaani mtu anam’baka na akimaliza  anamlawiti papo hapo kitendo ambacho watoto hao hukutwa wameharibika vibaya sana sehem za siri na wakati huohuo sehem za haja kubwa” Alisema Eliza.

Akitolea mfano Dr. Eliza alisema “kwa mfano hivi majuzi tu hapa agost 29 mtoto wa mwaka mmoja na miezi 9 tu alibakwa na baba yake na wakati huo huo akamlawiti hali iliyofanya kuchanika vibaya sehem ya haja kubwa na ndogo na kuwa kitu kimoja.....hebu fikiria hata wewe ni maumivu kiasi gani amepata mtoto huyo? Alimalizia Eliza kwa swali.

Kwa upande wa baadhi ya wazazi wa watoto waliofanyiwa vitendo hivyo wakizungumza na mwandishi wa habari hizi hospitalini hapo walisema kuwa vitendo hivyo vinazidi kushamiri kutokana na wahusika wa vitendo hivyo kutokupewa adhabu kali wakibainika kuhusika na vitendo hivyo.

 

Mmoja wa mama wa mtoto aliyefanyiwa vitendo hivyo, Helena Jeseph mkazi wa Siwandeti kata ya Ngateu iliyoko wilayani Arumeru alisema kuwa mtoto wake Ester alifanyiwa kitendo hicho cha ubakaji na Adam Daudi mkazi wa eneo hilo hilo la Ngateu lakini hakuna hatua yoyote inayochukulia dhidi yake kutokana na wazee wa mila kumkingia kifua kwa madai ya kumaliza kimila.

“Mimi mtoto wangu alibakwa na kijana wa hapo mtaani kwetu anaitwa Adamu ambae pia aliwahi kuwabaka watoto wengine wa hapo hapo mtaani kama wanne hivi tangu mimi nimfaham lakini cha kushangaza hakuna hatua yoyote ya kisheria inayochukuliwa dhidi yake kwani akipelekwa polisi wazee wa mila wanaenda kumtoa kwa madai ya kuja kumaliza nyumbani lakini akirudi huwaonga wazee wale pombe na nyama na kesi hiyo kuishia hapo, mzigo unabaki kwa familia kumuuguza mtoto Yule” Alisema Helena, na kuongeza,

“Kama inavyofahamika sisi wamasai bado kuna mfumo dume kama kwani wazee wa mila wakikubali kitu wewe kama  mama huwezi kupinga, hivyo unabaki unanyamza na kumuuguza mtoto wako kwa gharama zako mwenyewe huku wabakaji wakiendelea kukutishia kuwa ukiendelea kumfuatilia atakubaka hata wewe yaani mimi na kujitamba kuwa hakuna utakapompeleka....., mfano mzuri ni huyu Adam wa mtaani kwetu amebaka watu wazima na watoto zaidi ya wane lakini hakuna cha kufanya.” Alimalizia Helena huku akibubujikwa na machozi.

Akielezea tukio la kubakwa kwa mwanae, alisema kuwa agost 25 alimtuma mwanae dukani akiwa na wenzake majira ya mchana ambapo njiani alikutana na huyo Adam na kumwita mtoto huyo wa miaka 9 kwa madai ya kutaka kumtuma dukani, ambapo alimchukua mtoto huyo hadi mashamba ya kahawa yaliyopo maeneo hayo kwa madai ya kwenda kumchukulia fedha na kumuahidi kumpa pia mtoto huyo fedha za kununua pipi lakini baada ya kufika katikati ya mashamba hayo alimlazimisha mtoto huyo kuvua nguo na kulala chini chali huku akiwa amemziba mdomo ambapo alijipaka mafuta aina ya baby care sehem zake za siri na na kuanza kumwingilia mtoto huyo bila huruma hadi kumchana vibaya sehem zake za siri.

Alisema kuwa mbali na kijana huyo kuhusika na matukia hayo yote, lakini bado yuko mtaani akijitamba ambapo akikamtwa na polisi kwa ajili ya kupelekwa mahakamani wazee humtoa mahabusu ambapo huja kuomba radhi  na kuahidi kutoruia tena kwa madai shetani ndio alimwingilia lakini baada  mda hurudia tena hali iliyokuwa kama mazoea kwake.
 
 
 
Mwandishi wa habari hizi Katika  kutaka kujua hatua za Jeshi la polisi  juu ya kudhibiti vitendi hivyo hasa kwa wahusika ambao bado wako mitaani wakitamba kutoacha ubakaji, Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberetus Sabas alisema kuwa vitendo hivyo ni vya kawaida hivyo vitafanyiwa kazi kwa mujibu wa ratiba kwani bado havijakithiri.
“Huo ni uhalifu mdogo tu ambao ni wa kawaida sana ukilinganisha na ukubwa wa mkoa wetu,hivyo vitafanyiwa kazi kwa mujibu wa ratiba wala haina shida hilo,”Alisema Kamanda Sabas.
Hata hivyo majibu hayo yaliacha maswali mengi yanayokosa majibu juu ya uhalifu wa ubakaji kuwa wa kawaida wakati wahusika wakiendelea kunyanyasika na kuteseka na zaidi ya yote kuathirika kisaikolojia lakini mbaya zaidi kuambukizwa magonjwa ya zinaa ikiwemo UKIMWI, huku watanzania wakiambiwa Tanzania bila UKIMWI inawezekana, je kwa mtoto huyu anaebakwa na kulawitiwa aambiwe nini?
 
 
 

0 comments:

Post a Comment