.

.
Saturday, September 7, 2013

10:52 PM


WANAFUNZI wawili wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari matombo katika wilaya ya morogoro wamejeruhiwa, na wengine watatu kunusurika, baada ya kulipukiwa na kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu, wakati wakitoka shuleni.
 
Wanafunzi hao waliojeruhiwa katika sehemu mbalimbali za miili yao ni  Luciani Juma (14) na Anthonia Charles (15), wakazi wa kijiji cha Konde, Tarafa ya Matombo wilayani Morogoro, ambapo Luciani aliyelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.
 
akizungmza na waandishi wakati wakipata matibabu, kuwa walipatwa na tukio hilo wakati wakitokea shuleni, ambapo njiani  walikutana na kitu mfano wa balbu ya tochi ambacho hata asubuhi wakati wa kwenda shule walikiona na kukipuuza, na mmoja wawanafunzi alikirushia ganda la muwa aliokuwa akila, na kililipuka na kutoa mshindo mkubwa.
 
Daktari anayemtibu Lucien katika wadi namba moja ya hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro, aliyejulikana kwa jina moja Dk. Francis amesema majeruhi huyo anaendelea vizuri, na amepata majeraha katika sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo sehemu za siri, kwenye paja na sehemu ya nyonga na kwamba katika maeneo hayo walifanikiwa kutoa vitu mfano wa chuma.
 
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro John Laswai, amethibitisha kujeruhiwa kwa wanafunzi hao, ambapo majeruhi Anthonia ametibiwa na kuruhusiwa na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi kubaini kitu kilichowajeruhi wanafunzi hao, ambacho kilitoa mshindo mkubwa na mtawanyiko wa vyuma, kama kilikuwa ni bomu ama vinginevyo.

0 comments:

Post a Comment