.

.
Thursday, September 12, 2013

1:19 PM


ROBIN VAN PERSIE amemfunika gwiji wa soka wa Uholanzi Denis Bergkamp kwa kufunga mabao mengi katika listi ya washambuliaji wa nchi hiyo walioifungia The Oranje mabao mengi.

Van Persie anakaribia kuwa mfungaji bora wa muda wote kwa taifa lake.

Mabo yake mawili aliyofunga jzui yamefanya ampite mchezaji mwenzie wa zamani wa Arsenal Dennis Bergkamp mwenye mabao 38, wakati Van Persie akiwa na mabao 38.

Van Persie sasa anashika nafasi ya pili nyuma ya Patrick Kluivert, ambaye ana mabao 40, na sasa kwa hakika ni suala la muda tu kabla ya Van Persie kumfikia na kumpita mshambuliaji huyo wa zamani wa FC Barcelona.

Mshambuliaji huyu wa Manchester United alifunga goli la kwanza akiwa na jezi ya Uholanzi mnamo mwaka 2005, alipoweka kimiani goli la nne katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Finaldn katika michuano ya kugombea kufuzu kucheza kombe la dunia 2006.

0 comments:

Post a Comment