.

.
Saturday, December 28, 2013

10:32 AM
Mafundi wakikamilisha hatua za mwisho jana.
Makaburi ya watu watatu waliouawa na mabomu May 5,mwaka huu.
Maandalizi ya vya mwilini.
Mafundi wakijenga eneo lilipotua Bomu kama kumbukumbu ya kudumu iliyopoteza maisha ya watu na kujeruhi.
Balozi wa Baba Mtakatifu nchini,Fransisco Padilla hatimaye leo amezindua Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Olasiti ambalo lilikua lizinduliwe May 5 mwaka huu lakini zoezi hilo lilisitishwa baada ya kutokea shambulio la bomu la kutupwa kwa mkono lililosababisha watu 3 kufariki dunia na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa.
Uzinduzi huo uliofana kwa shangwe na furaha baina ya waumini wa dhehebu hilo na wakazi wa Arusha kwa ujumla ulifanikiwa kuhudhuriwa na maaskofu kutoka sehem mbalimbali katika pembe za nchi ya Tanzania waliokuwa wakimpongeza balozi Fransisco kwa ujasiri wake wa kurudi kwa kazi hiyo.
   

0 comments:

Post a Comment