.

.
Sunday, January 6, 2013

7:45 AM

Watanzania wametakiwa kujenga mazoea ya kuwasaidia watoto yatima badala ya kuwatumia kujipatia kipato au kuwadhulumu mali zao walizonazo ikiwemo zile zilizoachwa na wazazi wao.





Rai hiyo imetolewa na diwani wa kata ya sokon one mh, Michael kivuyo alipokuwa akiongea na wamiliki na walezi wa watoto yatima waishio vituoni pamoja na watoto hao zaidi ya 100 kwenye ghafla fupi ya kupata chakula cha mchana na watoto waishio katika vituo vya watoto yatima vilivyoko katika kata ya sokon one.





Kivuyo amesema kuwa watu wengi kwa sasa hawana hata hofu ya Kimungu kwani badala ya kuwasaidia watu wenye mahitaji kama yatima baadhi yao wamekuwa wakiwatumia kujipatia kipato kwa kuanzisha vituo vya watoto yatima kwa lengo la kujipatia kipato kutoka kwa wadau kwa madai ya kuwasaidia watoto hao lakini kuhutumia misaada hiyo kwa manufaa yao binafsi.





Aliongeza kuwa si hao tu pia wako baadhi ya watu au hata ndugu ambao wamekuwa wakiwanyanyasa watoto yatima walioachwa na wazazi wao baada ya kutangulia mbele za haki kwa kuwanyanganya mali walizoachiwa na kujimilikisha wao na kuwaacha watoto hao wakihangaika bila chochote wala msaada.





Mbali na hilo Kivuyo pia aliwageukia watoto hao yatima na kuwataka watoto hao waliobahatika kuwepo kwenye vituo vya watoto yatima na kulelewa vizuri hatimaye kuweza hata kusomeshwa wasijinyanyapae kuwa hawawezi kufanya vizuri kwa kutokuwa na wazazi badala yake wajitahidi kufanya vizuri katika masomo yao ili waweze kufaulu hatimaye kushika nafasi mbalimbali serikalini au hata nafasi binafsi ili kuwasaidia wenzao baadae.





Kabla ya kuombea chakula hicho kilichoandaliwa na diwani kwa ajili ya watoto yatima, mch, Julius Laizer alisisitiza kwa kuwataka watu kuwa na hofu ya Mungu ya kuwadhulumu yatima na wajane mali zao badala yake wateke baraka kwa kuwasaidia kuzitetea mali hizo na hata kujenga mazoea ya kutenga bujeti zao na  kuwasaidia watu hao ili Mungu aweze kuwabariki na wao mara dufu.





Adha hafla hiyo iliyoandaliwa na familia ya diwani wa kata ya sokon one ilifanyika katika kanisa la kipetekoste la Niavera  iliyoka katika kata ya sokon one, ilihudhuriwa na watoto yatima zaidi ya 100 waishio katika vituo 4 vya kata hiyo na wamiliki wa vituo vya watoto hao wakiwemo walezi na wageni wengine.

0 comments:

Post a Comment