.

.
Thursday, January 10, 2013

11:14 AM
DSCF7081
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh.Nyirembe Munassa akifungua mkutano.

Imeelezwa kuwa kukuwa kwa uchumi duniani hasa kwa nchi zinazo endelea kunategemea njia bora  za utunzaji wa mazingira kwa kuzingatia uzalishaji bora wa viwanda unaoendana na viwango vya kimataifa
Hayo yameelezwa jijini Arusha leo wakati wa mkutano wa viongozi wa kimataifa wanaoshughulikia viwango vya maswala ya mazingira duniani,ambapo mgeni rasmi katika mkutano huo alikuwa  mkuu wa wilaya ya Arumeru Mh.Nyirembe Munassa
Nyirembe Munassa amesema nchi za dunia ya tatu ziko katika hali mbaya zaidi kutokana na uwezo duni wa kupambana na athari za mabadiriko ya tabia nchi
Nae mwenyekiti wa mkutano huo Prof. Robert Page amesisitiza kuanzishwa  kwa  mkakati madhubuti wa kupunguza athari hizo kutokana na kwamba maendeleo ya kiuchumi yoyote hutegemea kwa kiasi kikubwa mazingira yaliyo tunzwa vizuri
Mkutano huo ni wa siku mbili unaoshirikisha wataalamu wa viwango na wadau wa mazingira duniani, pamoja na mambo mengine utajadili mpango wa kuwa na  teknolojia safi katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali duniani kote

0 comments:

Post a Comment