.

.
Friday, January 11, 2013

12:29 PM
NUSU ya watu wanaotumia kondomu kwa ajili ya kujikinga na mimba ama magonjwa ya zinaa, hawajui namna ya kuitumia mipira hiyo, utafiti umeeleza.
Utafiti huo mpya ulifanywa na Dk Stephanie Sanders wa Taasisi ya Kinsley inayohusika na Utafiti wa Masuala ya Jinsia, Jinsi na Uzalishaji katika Chuo Kikuu cha Indiana.
Kwa mujibu wa utafiti huo uliofanywa katika nchi 14 ikiwamo Tanzania katika kipindi cha miaka 16 iliyopita kuanzia mwaka 1995 hadi 2011, watu wengi wamekuwa wakifanya makosa kwa namna mbalimbali katika kutumia kandomu ikiwamo uvaaji.
“Makosa yanayofanywa mara kwa mara na watumiaji wa kondomu ni pamoja na kuingiza kinga hiyo nusu katika uume wakati wa ngono au kuitoa kabla tendo hilo halijamalizika au kusubiri mpaka isinyae,” imesema sehemu ya utafiti huo.
Makosa mengine ni kutoacha nafasi katika ncha ya kondomu kwa ajili ya mbegu za kiume na kuzifungua vibaya katika pakiti yake.
Jambo hilo linalosababisha kucha kuzitoboa na hatimaye kupitisha mbegu au majimaji kwenda kwa mwanamke,” umeeleza utafiti huo.
Utafiti huo umeonyesha kuwa makosa mengine ni kuigeuza kondomu ndani-nje, kuihifadhi katika sehemu isiyostahili na kurudia kuitumia katika tendo lingine la ngono.
Kuivua vibaya: Asilimia 57 ya watu waliohojiwa, walikiri kuvua kondomu kimakosa baada ya tendo la ngono. Kati yao asilimia 27 walikuwa wanawake na asilimia 31 ni wanaume.
Pamoja na makosa hayo ya uvaaji wa kondomu, watafiti nchini India wanatarajiwa kufanya utafiti mwingine mkubwa kuhusu suala hilo kubaini sababu yake.
Watafiti hao waliamua kufanya uchunguzi baada ya kubainika kuwapo kwa wanaume ambao maumbile yao ni makubwa au madogo kuliko mipira hiyo ya kiume.
Hata hivyo, kondomu zinazopatikana nchini Tanzania hazitofautiani ukubwa.
Dk Sanders alisema makosa yanayofanywa wakati wa kutumia mipira hiyo yanachochewa na watumiaji wenyewe na kukosekana kwa msisitizo wa elimu ya namna ya kuzitumia kondomu hizo kutoka kwa watengenezaji au taasisi za Ukimwi.
Makundi tofauti yalijumuishwa katika utafiti huo wakiwemo wanandoa, wafanyabiashara ya ngono na wanafunzi wa vyuo.
Kati ya asilimia 17 na 51.1 ya watu walioulizwa maswali katika utafiti huo walikiri kuwa huingiza kondomu nusu katika uume wakati wa tendo la ngono.
chanzo :mwananchi

0 comments:

Post a Comment