.

.
Monday, April 15, 2013

10:38 AM
Huu ni msiba wa tatu katika muda wa mwezi mmoja kwani mwishoni mwa mwezi jana, Wakili na Mfanyabiashara maarufu mkoani Arusha, Nyaga Mawalla alifariki dunia, ikiwa ni siku moja tagu kufariki ghafla kwa mfanyabiashara mwingine wa madini wa mkoani humo, Henry Nyiti.
Ndege aina ya Cessna  5H-QTT  ikiwa imeanguka eneo la Kisongo,  karibu na Uwanja wa Ndege Arusha  juzi jioni, baada ya kugonga mti wakati ikijiandaa kutua  na kusababisha kifo cha mmiliki wake na aliyekuwa rubani, Bob Sambeke(katika picha ndogo juu).
ARUSHA/MOSHI.  
Kwa mara nyingine, Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha imetikiswa, kutokana na kifo cha mfanyabiashara maarufu katika mikoa hiyo, Joseph Sambeke (49) maarufu kama Bob Sambeke.

Bob Sambeke alifariki dunia juzi jioni baada ya kuanguka na ndege ndogo aliyokuwa akiiendesha, kilomita moja kutoka Uwanja wa Ndege wa Arusha wakati akitokea mkoani Kilimanjaro.

Huu ni msiba wa tatu katika muda wa mwezi mmoja kwani mwishoni mwa mwezi jana, Wakili na Mfanyabiashara maarufu mkoani Arusha, Nyaga Mawalla alifariki dunia, ikiwa ni siku moja tagu kufariki ghafla kwa mfanyabiashara mwingine wa madini wa mkoani humo, Henry Nyiti.

Ndege ya Sambeke aina ya MT 7- namba 5H-QTT ilianguka saa 12.40 jioni baada ya bawa lake kugonga mti katika eneo la Magereza linalopakana na uwanja huo.

Alijeruhiwa na baadaye alifariki akiwa njiani wakati akiwahishwa hospitalini na askari wa Magereza ambao wanaishi katika kambi alipoanguka. Mazishi yake yamepangwa kufanyika Alhamisi eneo la Karanga, Moshi.

Meneja wa Uwanja wa Ndege Arusha, Ester Dede alithibitisha jana kutokea kwa ajali hiyo, na kueleza kuwa taarifa za awali zinaonyesha ndege hiyo ni mali ya marehemu Mawalla ambaye alikuwa mbia wa biashara na Bob Sambeki na imesajiliwa kupitia Kampuni ya Quality Tours & Travellers.

Hata hivyo, Wakili Alex Msando, ambaye pia alikuwa mshirika wa Mawalla, aliliambia gazeti hili kuwa Sambeke alikuwa ameinunua ndege hiyo kutoka kwa marehemu.

Dede alisema ndege hiyo, ilianguka mita 200 kutoka njia namba 8 ya kuruka ndege katika uwanja huo ikitokea Kilimanjaro, katika dakika 15 za muda wa nyongeza wa matumizi ya uwanja huo.

Alisema ndege hiyo ikiongozwa na rubani Bob Sambeki ina uwezo wa kubeba watu wanne akiwamo rubani. 

Baadhi ya walioshuhudia tukio hilo, walisema kabla ya kuanguka ndege hiyo, ilikuwa ikiyumba na iligonga mti mkubwa katika moja ya mabawa yake na kupoteza mwelekeo.

Mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo, Novis Kayombo alisema kwamba aliona ndege hiyo ikigonga mti na kuyumba, kisha kudondoka chini na ndipo askari wa magereza walipojitokeza kutoa msaada. 

Kayombo alisema Sambeki alikuwa peke yake na alijeruhiwa kichwani.
Kifo chake ambapo taarifa za kifo chake zilianza kuzagaa kwa kasi juzi saa 2:00 usiku na kusababisha taharuki katika Miji ya Moshi na Arusha. 
Chanzo:mwananchi 
Kwa taarifa za awali za familia yake wamesema kuwa mwili wa marehem Sambeke utaagwa nyumbani kwake njiro siku ya juma tano saa saba mchana ambapo mwili wake utasafirishwa hadi Moshi ambapo ndipo shughuli za maziko zatafanyika huko.
Bertha blog inatoa pole na kuwatia moyo familia ya Joseph Sambeke, ndugu na jamaa wa marehem Sambeke
BWANA AMETOA,  BWANA  AMETWAA JINA AKE LIHIMIDIWE
AMINA
 

0 comments:

Post a Comment