.

.
Tuesday, May 14, 2013

4:19 AM

Mtuhumiwa Bomu Kanisani Arusha, Victor Ambrose Calist (20).
Na Bertha Ismail-
Arusha
 

Jeshi la polisi mkoani Arusha,  limemfikisha mahakamani mtuhumiwa wa ugaidi, Victor Ambros Kalist (20) mwendesha boda boda mkazi wa Kwa Morombo jijini hapa na kuwaachia huru Raia wanne kutoka nchi za falme za kiarabu ambao waliingia nchini Mei 4 mwaka huu,baada ya kubaini kuwa hawausiki na tukio hilo.
Akisoma mashitaka mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya , Arusha, Devota Kamuzola, mwendesha mashitaka wa serikali Zacharia,akiwasaidiwa na Haruna Matagane na SC Ndomba,alisema kuwa  mshitakiwa, Ambros anashitakiwa kwa makosa 21 yakiwemo matatu ya kuuwa na 18 ya kujaribu kuuwa .
Alisema kuwa mnamo Mei 5 mwaka huu huko maeneo ya Olasiti majira ya saa4.30 katika kanisa la Mt.  Joseph mfanyakazi, Ambros aliua watu watatu, Partisia Joakim,Regina Lining’o na James Kessy kinyume cha kifungu namba 196 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa maboresho mwaka 2002.
Akisoma shtaka la pili alisema Ambros alijaribu kuuwa watu 18 kinyume cha kifungu namba 211(a) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa maboresho mwaka 2002.
Aidha katika shauri hilo la jinai namba 18 ya mwaka 2013, mshitakiwa hakutakiwa kujibu chochote na kurudishwa rumande hadi kesi yake itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Akizungumzia kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa huyo kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas alisema kuwa jeshi la polisi kwa kushirikiana na ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali limejiridhisha na ushahidi walioupata na kumfikisha mahakani.
Hata hivyo kamanda Sabasi aliwataja raia wanne wa kigeni toka nchi za falme za Kiarabu  (UAE) walioachiwa huru na kurudishwa makwao kuwa ni  Abdul Azizi Mubarak (30)ambae ni mfanyakazi wa mamlaka ya mapato katika falme hizo na mwingine ni Fouad Saleem Ahmed Al Hareez AL Mahri (29) ambae ni mfanyakazi kikosi cha zima moto.
Wengine ni Saeed Abdulla Saad (28) ambae ni skari polisi kitengo cha trefik karika falme hizo pamoja na Raia mmoja wa Saudi Arabia Al-Mahri Saeed Mohseens (29).
Aidha aliendelea kueleza kuwa uchunguzi wa kina unaofanywa na timu ya upelelezi ukihusisha taasisi zingine za upelelezi FBI pamoja  na Interpol kuhusiana na mlipuko wa bomu bado unaendelea kuwahoji watuhumiwa wengine kati ya 9 waliokuwa wanashikiliwa.

0 comments:

Post a Comment