.

.
Monday, May 27, 2013

2:39 AM

Na Juma Mtanda, Morogoro

MKUU wa wilaya ya Mvomero, Anthony Mtaka amezindua mradi wa maji na usafi wa mazingira kwa shule za msingi Mlali na Vitonga wenye thamani ya Sh72.7milioni ukiwemo wa uvunaji wa maji ya mvua katika kata ya Mlali mkoani Morogoro. 
Mradi huo umetekelezwa na shirika la Environmetal Conservation, Water Sanitation and Aids Control Organization (EWACO) kwa ufadhili wa shirika la WaterCan na wananchi wa vijiji vya Mlali na Vitonga. 

Akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara kwa nyakati tofauti katika vijiji vya Mlali na Vitonga, Mtaka alisema kuwa shirika la EWACO limeondoa moja ya kero ya muda mrefu ya shule za msingi Mlali na Vitonga kwa kujenga miradi hiyo yenye thamani ya Sh 72.7 milioni.

Alisema kuwa ili miradi hiyo iweze kuendelea kudumu ni lazima walimu, wanafunzi na wakazi wa eneo hilo kutunza miundombinu yake ili iendelee kuleta faida kwa walengwa. 

Shirika Ewaco  linapwa kuigwa na mashirika mengine kutokana na utendaji wao kwani thamani ya fedha iliyotajwa inafafana na thamani ya miradi iliyotekelezwa. Alisema Mtaka. 

Naye Mratibu wa Shirika hilo, Stanley Shekigenda alisema kuwa shirika hilo imetekeleza miradi miwili ya uvunaji wa maji ya mvua na ujenzi wa vyoo  katika shule za msingi Vitonga na Mlali kwa ufadhili wa shirika la WaterCan pamoja na kushirikiana na wananchi. 
Shekigenda alitolea ufafanuzi wa fedha zilizotumika kwenye miradi hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa shule ya msingi ya Mlali uliogharimu Sh46,6 milioni na shule ya Vitonga kiasi cha Sh26.1 milioni mbali na fedha kutoka EWACO pia wananchi wa Mlali imechangia kiasi cha Sh4.9 milioni na wale wa kijiji cha Vitonga wamechangia Sh2 milioni. 

Shekigenda alisema kuwa ujenzi wa mantaki mawili ya uvunaji wa maji ya mvua yenye ujazo wa lita 110,000 yaliyojengwa katika shule ya msingi ya Mlali na matundu 20 ya vyoo vya walimu na wanafunzi, wakati shule ya msingi Vitonga likijengwa tanki la lita 56,000 na ujenzi wa matundu 17 ya vyoo kwa walimu na wanafunzi. 
Mwisho…  

0 comments:

Post a Comment