.

.
Saturday, May 25, 2013

2:22 AM
Na Bertha Ismail -Arusha

Katika hali ya kuhakikisha ugonjwa wa kupinda miguu unatokomezwa kabisa hapa nchini, chuo cha mafunzo kwa watu wenye ulemavu kimewapa madaktari wa mifupa mafunzo ya wiki 2 ya namna ya kutibu ugonjwa huo bila opereshen hasa kwa watoto wadogo.

Hayo yameelzwa na mratibu wa mafunzo hayo, Grace Ayoo alipokuwa akizungumza na  waandishi wa habari mapema jana kwenye mafunzo hayo yalijumuisha madaktari wa mifupa kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini, yaliyofanyikia katika chuo cha mafunzo cha watu wenye ulemavu kilichoko USA river wilayani Arumeru Mkoani Arusha.

Alisema Mpango huo unaodhaminiwa na watu kutoka ujerumani, umefanikiwa kuwanyoosha miguu watoto zaidi ya 125 waliokuwa wamepinda miguu kutoka sehem mbalimbali hapa nchini katika chuo hicho hapo huku wakitarajia kusambaza huduma hiyo katika wilaya mbalimbali mkoani Arusha na baadae hata nchi nzima.

Grace alisema kuwa pamoja na juhudi za kutokomeza ugonjwa huo kwa watanzania lakini bado serikali ya Tanzania imekuwa haiko tayari kupongeza juhudi hizo kwa kuwasapoti kwa baadhi ya vifaa vya kutolea huduma ikiwemo pamba na P.O.P wakati wanaonufaika ni watanzania na kuongeza nguvu kazi ya taifa badala yake wanaosapoti kwa nguvu zate ni wajerumani.

Amesema kuwa kwa sasa wagonjwa ni wengi wanaojitokeza kutibiwa ugonjwa wa kupinda miguu, huku Iringa ikingoza hivyo kwa sasa wanataka kufungua tawi mkonia Iringa kuwasogezea wananchi hao huduma hii tofauti na sasa wanakuja hadi Arusha kufuata huduma hiyo.

Aidha alisema kuwa hadi sasa hawajui chanzo halisi cha ugonjwa huo ambapo bado wanaendelea kufanya utafiti kubaini na kutoa wito kwa jamii  kutohusisha ugonjwa huo wa ulemavu wa kupinda miguu na imani za kishirikina kama ilivyo sasa kwani ni ugonjwa wa kurithi na kutoka kwa mzazi mmoja au wote wawili ambo pia unatibika.

Kwa upande wake mwakilishi  wa wafadhili hao kutoka ujerumani Dr. Trine Heim alisema ugonjwa huo umekuwa kwa kiasi kikubwa hapa Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania.

Akielezea sababu za wao kufadhili mpango huo, alisema kuwa ujerumani wamefanikiwa kuutokomeza ugonjwa huo kwa kiasi kikubwa hivyo kuamua kusaidia ma watu wengine wakiwemo  watanzania lengo ikiwa ni kuutokomeza ugonjwa huo hapa Afrika.

Aliongeza kuwa kwa sasa mpango huo unaenda taratibu na kushindw a kufanikiwa kwa wakati kutokana na kulemewa na idadi kubwa ya wagonjwa huku serikali ya Tanzania ikishindwa kuusapoti mpanngo huo ili ulete tija kwa watanzania wengi zaidi kwa mda mchache.
 


0 comments:

Post a Comment