.

.
Monday, May 27, 2013

2:47 AM
Na Bertha Ismail-Arusha
Wananchi wa kitongoji cha Engutukoiti kilichoko katika kijiji cha Losinoni Kata ya Oldonyo sambu wilayani Arumeru mkoani Arusha wamemlalamikia mkuu wamkoa wa Arusha kwa kupuuza madai yao ya kupatiwa hadhi ya kuwa kijij.

Aidha wananchi hao waliandamana hivi karibuni hadi kwa mkuu wa mkoa kuwasilisha madai yao ya kudai hadhi ya kuwa kijiji ambapo walisikilizwa na katibu tawala wa mkoa wa Arusha Exvery Mwanga kwa niaba ya mkuu wa mkoa ambapo aliwataka wananchi hao warudi majumbani mwao na kuwaahidi mkuu wa mkoa angeenda kuwasilikiza siku ya jumatano may 21 mwaka huu.

Aidha wananchi hao waliamua kutii amri hiyo kwa kuwa na imani na mkuu huyo, ambapo ilipofika may 21 wananchi hao walikusayika kumsubiri mkuu wa mkoa kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa tisa mchana bila mafanikio ambapo mwenyekiti wa kitongoji cha Engutukoiti Lesikar Olobiis alijaribu kumpigia mkuu huyo na kuambiwa kuwa hana taarifa juu ya mkutano huo.

"Mimi baada ya kuona wananchi wamekusanyana hapa kutoka maeneo mbalimbali wakimsubiri mkuu wa mkoa bila mafanikio, niliamua kutafuta namba yake na kumpigia ambapo alisema kuwa yeye hana taarifa juu ya kikao hicho hivyo hawezi kuja" alisema mwenyekiti huo.

Aliongeza kuwa baada ya kujibiwa hivyo aliwaambia wananchi hao majibu aliyopewa hali iliyozua mtafaruku baina ya wananchi hao na baadhi yao kupandwa na jazba huku wakirusha maneno makali na kusema kuwa wamedhalilishwa na kudharauliwa na ofisi hiyo ya mkuu wa mkoa kwa kuahidiwa kusikilizwa jambo ambalo hawajatimiza.

mmoja wa wananchi Peter Senjore akiongea kwa jazba juu ya kutofika mkuu huyo alisema kuwawamekuwa na migogoro ya mara kwa mara kutokana na kutopewa haki yao ya kijiji lakini wakipeleka malalamiko hayo kwa viongozi husika akiwemo Mbunge wa jimbo hilo Godluck Ole Medeye  amekuwa nyuma kushughu;likia swala hilo hadi juzi kuamua kwenda kwa mkuu wa mkoa lakini matokeo yake ni kejeli na kudharauliwa.
|"Sisi wananchi wa kitongoji hichi tumekuwa kama si wananchi wa nchiii kwani kila tupatapo tatizo hakuna wa kushughulikia badala yake tumekuwa tukidharauliwa na kuonekana kama si kkitu, mfano mzuri ni juzi tulidai haki yetu hadi tukachoka bila msaaada na kuamua kulifikisha kwa mkuu wa mkoa tukidhani labda viongozi wetu hawafikishi matokeo yake ni kuwekwa hapa kama watoto wadogo haina shida Mungu atatutetea na kulipa, alisema mzee mmoja wa makam.

Mwananchi mwingine ni Selina Mohamed ambae kwa upande wake alilalamikia juu ya shughuli zake za kila siku alizoziacha ikiwemo kilimo, ufugaji na hata wengine kutokwenda kujitafutia riziri katika masoko kwa ajili ya kumsubiri mkuu huyo kuja kuwasilkiza na kutokomeza kero yao kubwa ya kupewa hadhi ya kuwa kijiji huku akisema kuwa baadhi ya watu wengine wametoka sehem za mbali lakini wameambulia kejeli za kudharauliwa.

Awali may 16 mwaka huu wananchi hao waliandamana hadi ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo kudai hadhi ya kupewa kijiji kwa madai ya kunyaswa na vitongoji vya jirani kwa kuwanyima huduma za kijamii kutokana na kitongoji hicho kupewa eneo kubwa na kufanikiwa kumiliki sehem ya malisho ya mifugo.

Katika maandamano hayo walipokelewa na katibu tawala wa mkoa Bwana Mwanga na kuwasilikiza huku akipokea makabrasha ya madai yao na kuwataka kurudi majumbani mwao kwani amekwishalifikisha na kuahidi kuwa mkuu kuyo angeenda kuwasilikiza tarehe 21 may hali ambayo imekuwa ndivyo sivyo kwa wananchi hao baaada ya kuambiwa na mkuu wa mkoa kuwa hana Taarifa hizo.

Pia ikumbukwe kuwa madai ya wananchi hawa kudai hadhi ya kuwa kijiji limekuwa la mda mrefu hali iliyosababisha migogoro ya hapa na pale baina ya kitongoji hicho na vingine vya jirani kwa ajili ya kugombe eneo hilo la malisho lililoko katika kitongoji cha Engutukoit na kusababisha watu wawili kupoteza maisha na maelfu ya mifugo kupotea huku kaya nyingi pia zikikosa mahala pa kuishi.


Baada ya mgogoro huo kupamba moto viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo mkuu wa mkoa wa Arusha alikwenda katika kata hiyo na kuzungumza na wananchi hao na kuahidi kufuatilia mpaka huo na kutatua tatizo hilo.
 
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo alipowasiliana na blog hii ya BERTHA BLOG juu ya madai hayo alisema kuwa yeye hana taarifa juu ya mkutano wala madai hayo hivyo aliyewaahidi amewatapeli tu na kuwataka waandishi na wananchi hao wakamuulize aliyesema maneno hayo.

0 comments:

Post a Comment