.

.
Wednesday, May 22, 2013

9:45 AM

WANANCHI Mkoani Mtwara wameamua kuingia barabarani na kuanza kufanya fujo zilizopelekea polisi kuanza kufyatua mabomu ya machozi kwa ajili ya kuwatawanya waandamanaji hao wanaoshindana na serikali kwa miezi kadhaa sasa.
Awali, wananchi wote mkoani Mtwara siku ya leo ilikuwa kufuatilia mambo ya Bunge yanavyokwenda, huku wakiwa na hamu ya kuona nini kitaamuliwa katika Bajeti ya Muhongo, wakitaka kuona mkoa wao unapendelewa zaidi kwa uwapo wa gesi.
Baada ya kuona bajeti hiyo ipo tofauti na dhamira yao, waliamua kurudi tena kwenye harakati zao kwa ajili ya kushinikiza malengo yao kwa serikali juu ya gesi.
Hadi sasa, mabomu yanaendelea kulipuliwa mjini hapa na wengi wasiokuwa na uwezo wa kushi
riki, hasa wazee wakiwa wamejichimbia majumbani mwao.
Sera ya mkoani Mtwara ni gesi kwanza, uhai baadaye, moja ya kauli mbiu zinazotumika kuwapa kiburi wananchi. Tangu kuzuiwa kufanyika kwa mikutano ya hadhara, wananchi wanatumia mbinu mpya ya kuhamasishana kwa njia ya meseji na vipeperushi na wakati mwingine kwa njia ya usafiri wa umma na kwenye maduka.
Taarifa zaidi zitaendelea kukujia ikiwa ni pamoja na maddhara ya vurugu hizo mkoani Mtwara.

0 comments:

Post a Comment