.

.
Monday, May 6, 2013

8:25 AM
ASKOFU mkuu wa kanisa katoliki jimbo kuu la Arusha ,Josephat Lebulu ameitaka serikali kutoa majibu ya msingi juu ya matukio ya kigaidi yanayozidi kuyaandama madhehebu ya Kikristo ikiwemo kuuawa kwa viongozi wa dini na weingien kujeruhiwa pamoja na kuchomwa kwa makanisa .

Kauli hiyo ameitoa katika hospitali ya Mkoa Mount Meru, wakati alipotembelea majeruhi wa bomu la kurushwa kwa mkono lililotokea jana wakati wa uzinduzi wa kanisa katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi lililopo Olasiti jijini hapa,ambapo watu wawili walifariki dunia na wengene zaidi ya 60 walijeruhiwa.

Alisema kumekuwepo ma mfululizo wa matukio ya kigaidi yaneyoelekezwa kwa makanisa pamoja na viongozi wa dini lakini serikali imeshindwa kutoa jibu kuhusiana na wahusiaka wa matukio hayo.

Aidha alisema kanisa halita lipiza kisazi ila halitaacha kusema juu ya uhalifu huo na kwamba serikali pamoja na vyombo vya  dola ikiwemo mahakama ndio wenye mamlaka ya kuuambia umma chanzo cha matukio hao pamoja na wahusika wa uhalifu huo.

“Wakatoliki hatuna desturi ya kulipa kisasi, najua hiyo ni kazi ya shetani imewaingia…tamko letu ni hilo hilo alilotoa Yesu Kristo la kutolipa ovu kwa uovu…ila hatuwezi kukaa kimya na kuruhusu matukio kama haya yaendelee,” alisema na kuongeza, “kwanini haya yanafanyika? Kwa nini Watanzania tunauana hovyo?
“Kama ni mwizi anatafuta nini kwa watu wanaosali na anawatupia bomu, huu ni ugaidi kabisa, sasa nani anayefanya na nani anayedhamini, ni wajibu wa serikali kutoa majibu wa mambo matukio haya,” alisema.
Akiongea na vyombo vya habari mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, (IGP), Said Mwema, amesema tukio la kurusha bomu kwenye mkusanyiko wa waumini lililotokea Jumapili katika Kanisa la Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Olasiti jijini hapa, halikupangwa na mtu na kutekelezwa na mtu mmoja pekee yake.

Alisema tukio hilo la kushtua na la aibu lazima litakuwa limepagwa na watu wengi na kwa uchunguzi unaoendelea kufuatia kukamatwa kwa watuhumiwa kuna kila uwezekano kuwanasa waliopanga na kuratibu tukio hilo.

IGP Mwema alisema hayo juzi jioni wakati akizungumza na wananchi waliofurika kwa wingi kwenda kuwajulia hali majeruhi wa tukio hilo katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru.

“Ni tukio la kushtua, kusikitisha, tumefika eneo la tukio na kuona hali halisi, tunashukuru kupata ushirikiano mzuri wa wananchi, napenda niwaeleze kwamba kuna kila dalili zote za kuwanasa waliopanga na kuratibu tukio hili.

“Tukio hili sio la mtu mmoja, wapo waliohusika katika kupanga, kuratibu, kushauri, kuchangia gharama na wale waliofanikisha. Dalili zinaonyesha tutawajua na kuwanasa waliohusika hivi karibuni,” alisema.

Akizungumza kwa niaba ya maaskofu wenzake waliowatembelea majeruhi hospitalini hapo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, alisema amesikitishwa sana na tukio hilo.

Askofu Mkuu Malasusa, pamoja na maaskofu wenzake walikuwa wameambatana na Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal, wakitokea mkoani Shinyanga, kwenye uzinduzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi Kusini Mashariki mwa Ziwa Victoria, na baada ya kusikia tukio hilo walikuja kuungana na wananchi wa Arusha na kuwapa pole.

Akizungumzia tukio hilo, Makamu wa Rais, Dk Bilal, alitoa pole kwa waumini, wakazi wa Arusha, majeruhi na ndugu zao na kwa uongozi wa kanisa, alisema serikali itawasaka wahusika usiku na mchana.

Naye Naibu  waziri wa Mali asili na utalii,Lazaro Nyarandu,pamoja na kutoa pole kwa majeruhi wa tukio hilo,alitoa msaada wa mablanketi 50 yenye thamani y ash,milioni 2.3 na kuahidi kutoa shilingi milioni 16 zitakazotolewa na mamlaka ya ya hifadhi Tanapa.

0 comments:

Post a Comment