.

.
Sunday, December 9, 2012

11:48 AM

Rais Jakaya Kikwete (pichani) amewataka Watanzania kujivunia na kuyaenzi mafanikio ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, yaliyopatikana tangu nchi ilipojipatia uhuru  wake mwaka 1961.
Akizungumza katika  maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa Tanzania Bara, uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salam leo, Rais Kikwete alisema yamekuwa tofauti na ya awali, safari hii yakihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kuu kutoka nchi 14 za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
Alisema mafanikio hayo yametokana na uvumilivu wa kisiasa ujengeka miongoni mwa Watanzania.
Viongozi mbalimbali wakiwa katika maadhimisha hayo kutoka kulia ni Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mama Maria Nyerere, Rais wa Msumbiji Mh. Armando Guebuza,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Gharib Bilal na Mzee Ali Hassan Mwinyi rais Mstaafu wa awamu ya pili
         Rais wa Msumbiji Mh. Armando Guebuza akipokewa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Said Meck Sadik mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Taifa.
 Kikwete alisema katika miaka 51 ya uhuru wa nchi hiyo, imekuwa katika utulivu na amani ambapo utulivu huo umekuwa chachu ya maendeleo katika jamii ya Watanzania.
Aidha, viongozi waliohudhuria maadhimisho hayo, Rais Kikwete amewataja kuwa ni pamoja Rais wa Jamhuri ya Congo (DRC), Joseph Kabange Kabila, Emilio Armando Guebuza, (Msumbiji), na Hifikepunye Pohamba (Namibia),  mbaye alishuhudia Tanzania Bara ikipata uhuru mwaka 1961 na Makamu wa Rais wa Zambia Guy Scott.
Wengine ni Makamu wa Rais wa Angola Manuel Domingos, Waziri Mkuu wa Rwanda, Pierre Au Moyen, Waziri Mukuu wa Swazland, Sibusiso Dlamini, Simba rashe na wengine.
Katika sherehe za maadhimisho hayo kulikuwa na burudani mbalimbali ikiwemo gweride la vikosi vya Majeshi, Halaiki ya watoto na ngoma za asili pamoja na kikundi cha Taifa cha ngoma za asili kutoka Rwanda.

0 comments:

Post a Comment