.

.
Friday, December 7, 2012

11:38 AM

Beki wa Zanzibar, Aggrey Morris akishangilia baada ya kuifungia timu yake bao la pili kwa penalti, Uwanja wa Mandela, Namboole katika Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge usiku wa leo. Zanzibar ilifungwa kwa penalti 4-2 na sasa itamenyana na Bara katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu Jumamosi.

Khamis Mcha 'Vialli' akishangilia baada ya kuifungia Zanzibar bao la kwanza

Adeyom Saleh Ahmed akimtoka beki wa Kenya, Joackins Atudo

Nadir Cannavaro ameruka na kipa wa Kenya

Mcha anapasua ukuta wa Kenya

Mcha Vialli kamlamba mtu chenga, kamuacha chini anaambaa

Suleiman Kassim 'Selembe' akipasua katikati ya msitu wa wachezaji wa Kenya

Kocha wa makipa wa Zanzibar, Farouk Ramadhan akimpa maelekezo kabla ya mechi kipa Mwadini Ally

Kikosi cha Zanzibar leo

Kikosi cha Kenya leo..

KILI STARS ILIPOKWAA KISIKI LEO NAMBOOLE, NI HUZUNI TUPU HADI HANS POPPE

Wachezaji wa Bara wakijadiliana baada ya kufungwa na Uganda katika mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge usiku wa leo kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala, Uganda. Uganda walishinda 3-0 na kutinga fainali, ambako watamenyana na Kenya Jumamosi.  

SURA ZA HUZUNI; Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe kulia akifuatilia mchezo kati ya Bara na Uganda. Kushoto wake ni Waandishi wa Habari wa Tanzania, Somoe Ng'itu juu na Zaituni Kibwana pembe ni kabisa Z.H.

Mwinyi Kazimoto akiwa amezibiwa njia kwa staili hadi ya kulala kama unavyoona hapo

Cheki ulinzi huo langoni mwa Uganda, Ngassa na Bocco peke yao wangefanya nini

Amri Kiemba anakokota ngoma
          

0 comments:

Post a Comment