.

.
Tuesday, December 18, 2012

11:12 AM

Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Hai Mh Freeman Mbowe Akiongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa
--
 Baadhi ya Maazimio
1.KIKAO cha kamati kuu kilikuwa cha kawaida ,hakuna jambo la dharula.
 
2.Mchakato wa katiba mpya usiathiri mabadiliko ya sheria nyingine kama mabadiliko ya sheria ya uchaguzi
 
3.Mwaka 2013,ni mwaka wa nguvu ya umma,hakuna kubembelazana na serikali.rais kikwete hajajibu madai ya CHADEMA kwa hiyo atashinikizwa.
 
4.sehemu ambazo CCM wanaogopa kuitisha uchaguzi,wanalazimishwa kuitisha uchaguzi.kata za arusha mjini,sengerema,nk.ziko 15
 
5.Uongozi wa KARATU wa CHADEMA umesimamishwa kwa muda mpaka chama kitakapokamilisha uchunguzi wake huko.wanasheria Marando na Prof Safari watachunguza kashfa za mtu mmojammoja huko karatu.,
 
      ..........xxx...........xxx..................xxx............
 


Aliyekua Mwenyekiti wa Tawi la Chadema UK, Chris Lukosi Aelezea Kisa Cha Yeye Kuondoka Chadema na Kurudi CCM...''


 Bw. Chris Lukosi
--
Leo hii nimeamua rasmi kurudi CCM, chama ambacho nimekifahamu kwa miaka 35 sasa.
  Nilijiunga na Chadema kwa matumaini niliyokuwa nayo kuwa ni chama kitakachomkomboa Mtanzania kutoka kwenye umasikini na kumfikisha kwenye level sawa na watu wa mataifa mengine kama Botswana , Namibia au hata baadhi ya nchi za Ulaya.
Niliamua haya baada ya kufuatilia yanayoandikwa kwenye vyombo vya habari kwa sababu mie binafsi kwa sasa naishi UK hivyo basi mambo mengi yatokeayo nyumbani huwa nayapata kwa kusoma magazeti na blogs mbali mbali.
Nilifanikiwa kukutana na Mheshimiwa Lema hapa London ambapo tukapanga mikakati ya kukijenga chama hapa UK na nikapewa jukumu la kufungua matawi nchi nzima na kuhamasisha Watanzania, kazi ambayo niliifanya kwa moyo mmoja. Pia nilichaguliwa kuwa mwenyekiti wa chadema UK.
Nimefanikiwa kuhamasisha watu wengi na baada ya miezi michache niliamua kwenda nyumbani kuona hali ilivyo. Niliyoyakuta ilikuwa tofauti na niliyokuwa nikiyasikia na kusoma.
NIMEKUTA BARABARA NZURI SIJAWAHI KUONA TOKA NIZALIWE NA ZINAENDELA KUJENGWA!
SHULE ZA SEKONDARI KILA KATA NA VYUO VIKUU VYA KUJICHAGULIA.
MAISHA YA WATANZANIA YAMEBADILIKA SANA - MIDDLE CLASS NI MAISHA YA KAWAIDA TU. VIJANA WENGI WAMEENDELEA TOFAUTI NA ZAMANI MPAKA UWE MCHAWI KIDOGO NDIO UWE TAJIRI. MIJI INAJENGEKA KWA KASI YA AJABU. UKIHARIBU KAZINI UTAWAJIBIKA .
 Na mengine mengi tu niliyaona mpaka nikaanza kujiuliza , hivi najiita mpinzani, NINAPINGA NINI?
 Kama ni maendeleo nayaona tena maendelo original Nikakumbuka msemo mmoja... “KWA NINI UHANGAIKE NA FOTOKOPI WAKATI ORIGINAL IPOO?”
Kwangu mimi CCM ni original na Chadema ni photocopy, tena copy iliyotolewa wakati mashine imekwisha wino . Mabadiliko ya kweli yatatokea ndani ya CCM na si kwingineko!
 Kuna mengi mazito yamenichefua Chadema lakini sitayasema leo. Juzi mwenyekiti wangu wa Taifa Mheshimiwa Mbowe alipita hapa UK, lakini, mpaka ameondoka hakutaka kuwasiliana na kiongozi yoyote wa Chadema hapa UK kitendo ambacho kiliniuma sana, kwani, niliona kama tumedharauliwa;
  BABA HUWEZI KWENDA SEHEMU WALIPO WANAO UKASHINDWA HATA KUWAPIGIA SIMU KUWAJULIA HALI.
Ni matumaini yangu kuwa uamuzi wangu utaeleweka. Kama tujuavyo, kila kwenye msafara wa mamba na kenge wamo, lakini naona kwenye msafara wa Chadema idadi ya kenge inazidi mamba.

0 comments:

Post a Comment