.

.
Thursday, November 29, 2012

9:44 PM

Ndikumana

Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba SC, Suleiman Yamin Ndikumana kwa sasa ndiye anaongoza kwa kufunga mabao katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge inayoendelea mjini hapa.
Ndikumana aliyewahi pia kucheza Norway na Uturuki, jana alifunga bao la tatu katika mashindano haya, akiichezea Burundi dhidi ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars. 
Sasa anamzidi kwa bao moja, John Bocco ‘Adebayor’ wa Kilimanjafo Stars.
Jumla ya mabao 17 hadi sasa yamefungwa katika mechi 16 za makundi yote matatu, zilizopigwa kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala.
Bocco anafungana na mshambuliaji mwingine wa Burundi, Christopher Nduwarugira, wakati wachezaji wengine ambao hadi sasa kila mmoja amefunga bao moja ni Farid Mohamed, Yussuf Ndikumana wa Burundi, Mohamed Jabril wa Somalia kwa penalti, Geoffrey Kizito wa Uganda, Yonatal Kebede Teklemariam, Haruna NiyonzimUganda, David Ochieng, Clifton Miheso na Jean Mugiraneza.
Kwa sasa Bocco anayechezea Azam FC ya Dar es Salaam, ndiye mshambuliaji pekee kwenye kikosi cha Bara, baada ya washambuliaji wengine, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemomkrasia ya Kongo (DRC) kuzuiliwa na klabu yao.
WAFUNGAJI CECAFA TUSKER CHALLENGE 2012
Suleiman Ndikumana   Burundi    3 (1 penalti)
John Bocco                  Tanzania  2
Chris Nduwarugira        Burundi   2
Yussuf Ndikumana       Burundi   1
Mohamed Jabril            Somalia   1(penalti).
Geoffrey Kizito              Uganda   1
Brian Umony                 Uganda   1
Yonatal Teklemariam     Ethiopia  1
Haruna Niyonzima         Rwanda  1
Jean Mugiraneza           Rwanda  1
David Ochieng               Kenya     1
Clifton Miheso                Kenya     1
Farid Mohamed              Sudan     1 

 .................xxx.............xxx.............xxx.................

KAZIMOTO, KAPOMBE HATARINI KUWAKOSA WASOMALI JUMAMOSI

Kazimoto
WACHEZAJI wawili wa Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, beki Shomary Kapombe na kiungo Mwinyi Kazimoto, walishindwa kumaliza mechi za jana, baada ya kuumia na sasa wako hatarini kuikosa mechi ya mwisho ya Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge dhidi ya Somalia, Desemba 1.
Wachezaji hao wa klabu ya Simba, wote waliumia kipindi cha pili na kutolewa, nafasi ya Kapombe ikichukuliwa na Issa Rashid wa Mtibwa Sugar nay a Mwinyi ikichukuliwa na Shaaban Nditi wa Mtibwa pia.
Wote walitoka wakichechemea, kuashiria wamepata maumivu makali kidogo na Kocha Mkuu wa Stars, Mdenmark, Kim Poulsen alisema ataangalia hali zao leo na kesho.
Kim pia alisema kwamba sasa imetosha kuzungumzia suala la washambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kama watajiunga na timu hiyo au la.
“Kwangu sasa lazima ifikie wakati iwe inatosha, sitaki kuwazungumzia tena wachezaji hao, waulizeni TFF,”alisema Poulsen baada ya kuulizwa kama mawasiliano na klabu yao kama yanaendelea juu ya kuombea ruhusa.
Mazembe imekataa kuwaruhusu wachezaji hao kwa sababu michuano ya Challenge haimo kwenye kalenda ya FIFA.
Kutokana na kukosekana kwa washambuliaji hao, Stars sasa inabaki na mshambuliaji mmoja tu kikosini, John Bocco ‘Adebayor’ wa Azam FC, ambaye Watanzania wanatakiwa kumuombea dua asiumie ili aendelee kuibeba timu yao ya taifa.
                  .............xxx.................xxx................xxx................

JOHN BOCCO AGEUKA LULU KUJMPALA, WATU WAANZA KUFIKA BEI

John Bocco

Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
SOKA ya nguvu aliyoonyesha mshambuliaji wa Tanzania Bara, John Bocco ‘Adebayor’ katika mechi mbili za Kundi B, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge zimemfanya awe lulu katika mashindano haya yanayoendelea mjini hapa.
Mawakala mbalimbali waliopo mjini Kampala wameanza kuulizia uwezekano wa kumtafutia timu Ulaya mchezaji huyo wa Azam, lakini uongozi wa timu ya Bara, Kilimanjaro Stars mjini hapa umewataka wawasiliane na klabu yake, Azam FC ya Dar es Salaam moja kwa moja.
Lakini pia kuna uwezekano klabu ya SuperSport United ya Afrika Kusini, iliyomfanyia majaribio Agosti mwaka huu ikamfikiria tena mchezaji huyo kutokana na kiwango kikubwa alichoonyesha hadi sasa kwenye mashindano haya.
Japokuwa hakufunga bao juzi kwenye mechi na Burundi, lakini kazi aliyoifanya wengi walikubali yeye ni mshambuliaji mzuri haswa kutokana na mfumo wa sasa wa kocha wa Stars, Mdenmark Kim Poulsen kumtumia peke yake mbele.  
Bocco ana mabao mawili kwa sasa, wakati mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Suleiman Yamin Ndikumana ndiye anayeongoza kwa mabao katika michuano hii.
Ndikumana aliyewahi pia kucheza Norway na Uturuki, juzi alifunga bao la tatu katika mashindano haya, akiichezea Burundi dhidi ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars. 
Jumla ya mabao 25 hadi sasa yamefungwa katika mechi 18 za makundi yote matatu, zilizopigwa kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala.
Bocco anafungana na mshambuliaji mwingine wa Burundi, Christopher Nduwarugira na mchezaji mwenzake wa Azam, Khamis Mcha ‘Vialli’ wakati wachezaji wengine ambao hadi sasa kila mmoja amefunga bao moja ni Farid Mohamed, Yussuf Ndikumana wa Burundi, Mohamed Jabril wa Somalia kwa penalti, Geoffrey Kizito wa Uganda, Yonatal Kebede Teklemariam, Haruna NiyonzimUganda, David Ochieng, Clifton Miheso na Jean Mugiraneza, Dadi Birori, Chiukepo Msowoya, Miciam Mhone, Patrick Masanjala, Amir Hamad Omary na Yosief Ghide.
WAFUNGAJI CECAFA TUSKER CHALLENGE 2012
Suleiman Ndikumana    Burundi    3 (1 penalti)
John Bocco                   Tanzania  2
Khamis Mcha                Zanzibar   2
Chris Nduwarugira        Burundi    2 
Yussuf Ndikumana        Burundi    1
Mohamed Jabril            Somalia    1(penalti).
Geoffrey Kizito              Uganda    1
Brian Umony                 Uganda    1
Yonatal Teklemariam    Ethiopia    1
Haruna Niyonzima        Rwanda    1
Jean Mugiraneza          Rwanda    1
Dadi Birori                    Rwanda    1
David Ochieng             Kenya       1
Clifton Miheso              Kenya       1
Farid Mohamed            Sudan      1
Chiukepo Msowoya      Malawi      1
Miciam Mhone              Malawi      1
Patrick Masanjala         Malawi      1
Amir Hamad Omary      Eritrea      1
Yosief Ghide                Eritrea       1(penalti).  

0 comments:

Post a Comment