.

.
Thursday, November 8, 2012

10:43 PM

 Na Mwajuma Ernest-Karatu
Serikali imetakiwa kutoa elimu ya sheria, kanuni na taratibu za umiliki wa ardhi kwa wananchi wake ili kuweza kupunguza au kumaliza kabisa tatizo la migogoro ya ardhi inayotokea mara kwa mara.


Rai hiyo imetolewa na mwanansheria wa kujitegemea Pascal hillu kwenye mdahalo wa umiliki wa ardhi  uliofanyika jumatatu wilayani karatu


Bwana Pascal alisema kuwa migogoro ya ardhi inayoendelea kwa sasa katika maeneo mbalimbali hapa nchini inasababishwa na wananchi kutotambua sheria na kanuni na taratibu za umiliki wa ardhi hivyo serikali imalize tatizo hilo kwa kutoa elimu hiyo kwa wananchi wake.


Alisema kuwa pamoja na mapungufu hayo pia serikali imekuwa ikiajiri watendeji katika sekta wasio na elimu


ya sheria za ardhi hali inayosababisha kutenda kazi kwa kuendekeza rushwa na kutoa maamuzi yasiyo ya haki na kusababisha migogoro zaidi kwa wale wanaoonewa


Akitolea mfano alisema kuwa rushwa imekuwa ikitawala sana hasa katika kutoa hati miliki ya ardhi ambapo watendaji husika hasa maafisa ardhi hudai rushwa la sivyo upatikanaji wa hati hiyo huwa ni ngumu na kuchukua mda mrefu.


Kwa upande wake katibu madahalo huo Best Ptrick aliiomba serikali kupitisha sheri ya kuweza kumshitaki afisa ardhi yeye ka ma yeye kuliko sasa ambapo anayefanya kosa ni mtendaji lakini serikali ndio hushitakiwa huku mtendeji akiendelea na utendaji mbovu ikiwemo kula rushwa.


Mdahalo huo ulioandaliwa na taasisi ya maendeleo isiyo ya kiserikali ya ijulikanayo kama KDA (Karatu Development Association) liliwahusisha watu mbalimbali wakiwemo wanafunzi, wanasiasa na viongozi wakiwemo wakiwemo wananchi.


Akizungumzia mdahalo huo katibu huyo bwana Best alisema kuwa wameamua kuitisha mdahalo huo kuwasaidia wananchi kuelewa sheria, na taratibu za umiliki wa ardhi baada ya kuona migogoro ya mara kwa mara katika jamii ya kugombea ardhi.


 Best alisema kuwa hata hivyo katika utoaji elimu hiyo wanakumbana na changamoto nyingi ikiwemo idadi ya watu wanaotarajia kutotimia kutokana na kutolipwa posho au baadhi yao kudharau mafunzo hayo.

0 comments:

Post a Comment