.

.
Thursday, November 8, 2012

10:26 PM
Mkuu wa usalama barabarani mkoani Arusha (RTO), Harison Mwakyoma akizungumzia ajali za barabara ofini kwake
Watu 152 wamefariki dunia na wengine 798 wamejeruhiwa  mkoani Arusha kufuatia ajali mbalimbali  zilizotokea mkoani  hapa kuanzia mwezi January hadi September mwaka huu.
Akizungumza na Bertha blog mkuu wa usalama barabarani mkoani Arusha, kamanda Harison mwakyoma alisema kuwa vifo hivyo vimetokana na ajali 1637 vilivyotokea kuanzia mwenzi wa kwanza mwaka huu hadi wa tisa ambapo kati ya ajali hizo 129 ndizo zilizosababisha vifo hivyo vya watu 152.
Aidha alisema kuwa mbali na vifo hivyo pia watu 1082 wamejeruhiwa kwenye ajali 798 zilizotokea kuanzia mwezi wa kwanza hadi wa tisa mwaka huu ambapo alisema kuwa kwa sasa ajali zimepungua kulinganishwa na ajali za mwaka jana.
Akitaja watu waliopoteza maisha mwaka jana alisema watu 198 walikufa katika ajali 164 huku watu 1305 wakijeruhiwa katika ajali 835.
Kamanda Mwakyoma alisema kuwa ajali kwa mwaka huu zimepungua kwa asilimia 84 ambapo jitihada hizo zimefanikiwa kutokana na mafunzo wanayoyatoa kwa sasa hasa kwa madereva wa bodaboda pamoja na opereshen ya kuwakamata wenye makosa ambao ndio wanaoongoza kwa kusababisha ajali za mara kwa mara pamoja na vifo vya kila siku.
Alisema kuwa kabla ya mafunzo kila siku walikuwa wakipata taarifa za ajali za bodaboda 2-3 lakini kwa sasa inapita siku 3-4 hawana taarifa yoyote ya ajali za barabarani hali ambayo ni mafanikio kwa jeshi la polisi kuwalinda wananchi na mali zao.
Mwakyoma aliongeza kuwa hadi sasa wamekwisha toa mafunzo kwa madereva zaidi ya 1000 wa bodaboda kuwawezesha kujua sheria, kanuni na taratibu za udereva hasa akiwa barabarani ambapo pia amewataka madereva hao kuhakikisha kuwa kila dereva anakuwa na kofia ngumu mbili(yaani element) kwa ajili ya dereva na mteja.
Sambamba na hilo kamanda Mwakyoma ameitaka jamii kuwa na mtazamo chanya wa kusaidiana katika kupunguza vifo kwa kutopanda vyombo vya moto kwa madereva wasio na mafunzo wala lesseni pamoja na kuhakikisha anapanda piki piki ambayo dereva atampa element ya kuvaa ambayo itasaidia ajali itokeapo kutokuumia au kufa.

0 comments:

Post a Comment