.

.
Monday, November 19, 2012

1:38 PM

Kesi ya madai inayowakabili waliokuwa madiwani wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema leo imehairishwa katika mahakama kuu ya kanda ya Arusha hadi hapo November  21 mwaka huu itakapo julikana hatima yao baada ya kushindwa kulipa fidia ya zaidi ya shilingi miolini 15 .


Kabla ya kuahirisha kesi hiyo hakimu mkazi mfawidhi ,Charles Magesa anayesikiliza kesi hiyo ,alisikiliza hoja za pande zote mbili,ambapo  wakili wa chadema, Method kimomogoro aliitaka mahakama iwachukulie hatua kali wahusika kwa kushindwa kulipa  fedha  hizo zilizoamuriwa na mahakama,April 10 mwaka huu.


Pia akimu kimomogoro aliiambia mahakama kwamba wadaiwa hao wamekuwa wasumbufu kwa kutaja kiwango kidogo cha kulipa ambacho ni kinyume na vipato vyao kwani katika mahesabu ya haraka inaonyesha kuwa kwa garama walizotaja wanaweza kulipa watatumia muda wa zaidi ya miaka 10 hadi kumaliza kumlipa mteja wake.


“muheshimiwa hakimu huoni kuwa kwa kila moja walivyojieliza kulipa kiasi hicho mara shilingili 15,000 kwa mwezi na wengine 25,000 watatumia mda mrefu mno,watakuwa wanatania maakama maana kunaambao wanawanavitega uchumi kibao huku wengine wakimiliki magari na wengine wakimiliki magari kwanini wasiuze au kukodisha na kama tukiwasikiliza si tutakuwa tunapotezea mda mahama “alisema kimomogoro


Kwa upande wa madiwani hao ambao ni Charles mpanda,John bayo ,robern ngowi ,Rehema Mohamed pamoja na Estomy Malla mmoja wa madiwani hao John Bayo akiongea mahakamani hapo alisema kwamba hawakatai kulipa lakini watalipa kutokana na vipato vyao na kuiomba mahakama ikubali kukubali kulipa viwango walivyovitaja.


Mara baada ya hoja za pande zote mbili kukamilika hakimu Magesa alihairisha kesi hadi hapo November 21 (kesho kutwa)ambapo ndipo maamuzi kamili yatatolewa.


Akiongea na waandishi wa habari nje ya mahakama method kimomogoro alisema kuwa Awali mteja wake chadema alipeleka mahakamani madai ya zaidi ya shilingi milini 2 9 lakini mahakama ilichambua na kuwataka walipwe shilingi 15,116,500 huku akibainisha kuwa wao wanasubiri mahamuzi ya mahakama apo kesho kutwa na iwapo wataamriwa walipwe watapokea .


“sheria ya mahakama inasema kuwa ukimpeleka mtu magereza unatakiwa umlipie hela ya chakula sasa wakishindwa kulipa tupo tayari kuwalipia chakula ili waende kusota magereza hadi pale watakapo lipa”alisema Kimomogoro


Aidha alibainisha kwamba iwapo mahakama itawahukumu kifungo fedha za chakula watawalipia na kuzijumlishia kwenye deni la mteja wake.



0 comments:

Post a Comment