.

.
Thursday, November 29, 2012

9:30 PM
Shangwe hizi zitaendelea kwa Uganda leo?
Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
MECHI za Kundi A, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge zinatarajiwa kufikia tamati leo kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini hapa.
Wenyeji na mabingwa watetezi, Uganda The Cranes wanatarajiwa kumaliza na Sudan Kusini, mchezo ambao utaanza saa 12:00 jioni, kabla ya hapo, kuanzia saa 10:00 jioni, Kenya Harambee Stars wataonyeshana kazi na Ethiopia.
Uganda wanaongoza Kundi A kwa pointi zao sita, wakifuatiwa na Ethiopia na Kenya, ambao kila mmoja ana pointi tatu. Sudan Kusini hawana pointi hata moja.
Ikumbukwe timu mbili za juu kutoka kila kundi, A, B na C zitafuzu moja kwa moja Robo Fainali, wakati kutoka makundi yote matatu, watatafutwa washindi wa tatu bora wawili, kukamilisha idadi ya timu za kucheza Nane Bora.
Kwa sababu hiyo, pamoja na kwamba Sudan Kusini wamepoteza mechi zote mbili za mwanzo, bado wanaweza kupigana kiume japo kugombea kupenya kama miongoni mwa washindi wa tatu bora.  
Kenya na Ethiopia bila shaka patachimbika leo- kwani timu zote zimefungwa na Uganda na zote zimeifunga Sudan Kusini- sasa leo itakuwa siku ya kujua nani nafuu kati yao.
Mechi nyingine za kukamilisha hatua ya makundi ya michuano hii, zitachezwa zote kesho za Kundi B na C.
MSIMAMO KUNDI A:
                      P   W  D   L    GF GA GD Pts
Uganda          2    2    0    0    2    0    2    6
Kenya            2    1    0    1    2    1    1    3
Ethiopia         2    1    0    1    1    1    0    3
Sudan Kusini 2    0    0    2    0    3    -3  0
MSIMAMO KUNDI B:
                     P   W  D   L    GF GA GD Pts
Burundi         2    2    0    0    6    1    5    6
Tanzania       2    1    0    1    2    1    1    3
Sudan           2    1    0    1    1    2    -1  3
Somalia         2    0    0    2    1    6    -5  0
MSIMAMO KUNDI C:
                     P   W  D   L    GF GA GD Pts
Zanzibar        2    1    1    0    2    1    1    4
Rwanda         2    1    0    1    3    2    1    3
Malawi           2    1    0    1    3    4    -1  3
Eritrea           2    0    1    1    2    3    -1  1
MECHI ZILIZOSALIA:
RATIBA KUNDI B:
Desemba 1, 2012:
Sudan v Burundi             (Saa 10:00 jioni)
Somalia v Tanzania        (Saa 10:00 jioni)
RATIBA KUNDI C:
Desemba 1, 2012:
Malawi v Zanzibar          (Saa 10:00 jioni)
Eritrea v Rwanda            (Saa 10:00 jioni)
VIWANGO VYA UBORA FIFA
NCHI                 NAFASI
Uganda             86
Malawi              101
Ethiopia            102
Sudan               102
Rwanda             122
Burundi             128
Kenya                130
Tanzania           134
Zanzibar            134
Somalia             193
Eritrea               192
Sudan Kusini    200
(Viwango hivi vimetoka mwezi huu)

0 comments:

Post a Comment