.

.
Tuesday, November 27, 2012

11:28 AM
 
Hayati Yasser Arafat
Mwili wa kiongozi wa zamani wa Palestina, Yasser Arafat, umefukuliwa kutoka kaburi lake liloko ukingo wa Magharibi mjini Rammala ili kuwawezesha kuufanyia uchunguzi kubaini iwapo aliuwawa kwa sumu.
Bwana Arafat alifariki dunia mwaka 2004 nchini Ufaransa baada ya kuugua kwa kipindi kifupi.
Maradhi yaliyopelekea kifo chake hayakubainika. Uamuzi wa kuufukua mwili wa Yasser Arafat katika kaburi lake lililoko ukingo wa Magharibi unafuatia makala ya televisheni iliyodai kupata mabaki ya madini ya kitonoradi aina ya Polonium kwenye nguo zake.
Wapalestina wengi wanashuku kwamba huenda Israel ilihusika katika kifo cha kiongozi huyo. Israel imekuwa ikikanusha shutuma hizo.
Uchunguzi wa mauaji dhidi ya Bwana Arafat umeanzishwa nchini ufaransa kufuatia ombi lililowasilishwa na mjane wake.
...............xxx........xxx.......xxx.....

Katu hatuondoki Goma'' wasema M23


Waasi wa M23 wamewalazimisha watu kutoroka mji wa Goma
Kiongozi wa waasi wa M23 ambao wiki jana waliuteka mji wa Goma Mashariki mwa DRC, wanasema katu hawataondoka Goma hadi serikali itakapotimiza matakwa yao.
Kiongozi wa kundi hilo, Jean-Marie Runiga alisema kuwa wapiganaji wake wataondoka mara moja ikiwa Rais Joseph Kabila, ataitikia matakwa yao ambayo ni pamoja na kuivunja tume ya uchaguzi.
Serikali ya Congo hata hivyo imepuuza matakwa hayo kama ya kipuuzi.
Uganda ambayo imekuwa ikipatanisha pande hizo mbili kwenye mkutano mjini Kampala, awali ilisema walikubali kuondoka Goma bila vikwazo.
Mnamo Jumamosi, serikali za nchi za Maziwa makuu ziliwapatia waasi hao makataa ya siku mbili kuondoka Goma.

0 comments:

Post a Comment